TANGAZO


Sunday, January 29, 2012

Vodacom yakabidhi madarasa 3 na madawati 100, Shule ya Msingi Ruvu

Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania, Mwamvita Makamba (kushoto), akipokea zawadi ya mbuzi toka kwa baadhi ya wazazi wa wanafunzi wa shule ya msingi ya Ruvu Darajani, iliyopo mkoani Pwani, mara baada ya kuwakabidhi rasmi vyumba vitatu vya madarasa na madawati 100 kwa ajili ya shule hiyo. Msaada huo uliotolewa na Vodacom Foundation na umegharimu zaidi ya shilingi Milioni 98.
 
 
 
Madarasa mapya yaliyokabidhiwa kwa  shule ya msingi ya Ruvu Darajani na Vodacom Foundation, iliyopo Mkoani Pwani jana.
 
 
 
Mkurugenzi wa Wizara ya Elimu kwa shule za Msingi, Zuberi Samataba, mwenye suti akiongea jambo na 0fisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania, Mwamvita Makamba,walipowasili katika shule ya msingi ya Ruvu Darajani iliyopo Mkoani Pwani kwa ajili ya kukabidhi msaada wa madarasa matatu na madawati 100, yaliyotolewa  na Vodacom Foundation katika shule hiyo na kugharimu zaidi ya shilingi Milioni 98.
 
 
 
Hili ndilo jiko la wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Ruvu Darajani, iliyopo mkoani Pwani.
 
 
 
Kikundi cha ngoma cha wazazi wa mkoa wa Pwani , kikitumbuiza wakati wa makabidhiano ya vyumba vitatu vya madarasa pamoja na madawati 100, vilivyokabidhiwa na Vodacom Foundation kwa ajili ya shule ya msingi ya Ruvu Darajani, mkoani Pwani. Msaada huo umegharimu zaidi ya shilingi milioni 98.
 
 
 
0fisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba, akikata utepe kuashiria uzinduzi wa vyumba vitatu vya madarasa pamoja na madawati 100 vilivyokabidhiwa na Vodacom Foundation kwa ajili ya shule ya msingi ya Ruvu Darajani iliyopo Mkoani Pwani.
 

No comments:

Post a Comment