TANGAZO


Saturday, January 28, 2012

Mkapa mgeni rasmi, mahafali ya DIT

 Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, akiwasili kwenye viwanja vya DIT kwa ajili ya kutunuku Shahada mbalimbali katika Mahafali ya Tano ya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), leo jijini. Kulia, aliyefuatana naye ni Mwenyekiti wa Taasisi hiyo, Fredrick Mwanuzi na kushoto ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Charles Kitwanga. (Picha na Kassim Mbarouk)


 Baadhi ya wahadhiri wa Taasisi hiyo, wakiingia kwenye viwanja hivyo, tayari kwa mahafali hayo ya Tano ya DIT leo.


Baadhi ya wageni waalikwa kutoka taasisi mbalimbali jijini, wakiingia kwenye viwanja vya mahafali hayo, nyuma ya mgeni rasmi, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, aliyeingia mwanzo viwanjani humo.


Mgeni Rasmi, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa (katikati), akiwa na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Charles Kitwanga (kushoto) na Mwenyekiti wa Taasisi hiyo, Fredrick Mwanuzi, wakiimba wimbo wa Taifa katika mahafali hayo. 


Mgeni Rasmi, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa (katikati), akiwatunuku wahitimu wa Stashahada ya Civil Engineering, katika mahafali hayo. Kushoto ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Charles Kitwanga na kulia ni Mwenyekiti wa Taasisi hiyo, Fredrick Mwanuzi.

 
  Baadhi ya wahitimu wa Stashahada ya Ujenzi (Civil Engineering), wakitunukiwa na mgaeni rasmi Rais mstaafu Benjamin Mkapa katika mahafali yao hayo, leo mchana.



 Mwanafunzi aliyefanya vizuri zaidi kuwazidi wenzake, Michael Christopher, akimpa mkono mgeni katika mahafali hayo, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa,


Mgeni rasmi wa mahafali hayo, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa (katikati), akipigapicha ya pamoja na wanafunzi waliofanya vizuri kwenye masomo yao, wakati wa mahafali hayo.


Mgeni rasmi wa mahafali hayo, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, akisindikizwa na Mwenyekiti wa Taasisi hiyo, Fredrick Mwanuzi (kulia anayezungumza naye) na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Charles Kitwanga (kushoto), wakati akiondoka kwenye viwanja vya mahafali vya DIT, mara baada ya kuyafunga rasmi mahafali ya Tano ya DIT, leo mchana. (Picha na Kassim Mbarouk)

No comments:

Post a Comment