TANGAZO


Tuesday, January 10, 2012

Rais Shein azindua Picha yake ya kuchorwa

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akifungua pazi kama ishara ya kuzindua picha ya kuchora kwa penseli, iliyochorwa na msanii Haji Simba (wa pili kushoto), wa kikundi cha Zan Artist cha Hurumzi, mjini Zanzibar. Picha hiyo, iliyofanana kabisa  na sura yake, ambayo inaonesha  anachuma karafuu, imechorwa kwa muda wa miezi miwili, sawa na siku 60, hadi kumalizika kwake. Wa tatu kulia ni Mshauri wa Rais, Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika, Abrahmani Mwinyi Jumbe na wapili kulia ni Mkurugenzi wa Kamisheni ya Utalii, Ali Khalil  Mirza. (Picha na Ramadhan Othman Ikulu)



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiiangalia  picha iliyochorwa na msanii, Haji Simba (kushoto), wakati alipoizindua picha yake hiyo ya kuchorwa leo mjini Zanzibar. (Picha na Ramadhan Othman Ikulu)


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akipata maelezo kutoka kwa msanii wa uchoraji, Haji Simba, aliyechora picha yake, akiwa anachuma karafuu, wakati alipozindua uchumaji wa zao la karafuu kisiwani Pemba.

No comments:

Post a Comment