TANGAZO


Sunday, January 7, 2018

NAIBU WAZIRI DKT. NDUGULILE AWASILI MKOANI KIGOMA KWA ZIARA YA SIKU MBILI YA KIKAZI

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (katikati), akisalimiana na Kaimu  Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Paul Chaote (kulia), alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Kigoma kwa ajili ya ziara ya siku mbili ya kikazi kufuatilia utekelezaji wa Sera mbalimbali zinazosimamiwa na Wizara yakekatika ngazi ya Mikoa na Halmashauri. kushoto ni Mwakilishi wa Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw. Julius Mbilinyi. 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinisa, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (katikati) akijadiliana jambo na Kaimu  Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Dkt Paul Chaote (kulia) na Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw. Julius Mbilinyi(kushoto) alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Kigoma kwa ajili ya ziara ya siku mbili ya kikazi kufuatilia utekelezaji wa Sera mbalimbali zinazosimamiwa na Wizara yake katika ngazi ya Mikoa na Halmashauri. (Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano-WAMJW)

No comments:

Post a Comment