Ndege iliyokuwa imewasili Toronto iliondolewa abiria baada ya kugongwa na ndege nyingine iyokuwa bila abiria wakati ikiondolewa kutoka lango la kutokea abiria.
Shirika la ndege la WestJet lilisema kuwa ndege yake aina ya Boeing 737-800, iliyokuwa na abiria 168 na wahudumu sita ilikuwa inasubiri kuegeshwa kwenye lango la kutokea abiria wakati iligongwa na na ndege ya shirika la Sunwing.
- Teksi ndege isiokuwa na rubani yazinduliwa Dubai
- Upepo wa injini ya ndege wamuua mwanamke New Zealand
- Marubani wafukuzwa kazi baada ya kuruhusu mtoto kuendesha ndege
Video ilionyesha moto karibu na mkia wa ndege ya Sunwing na abiria wa WestJet wakitiokea mlango wa dharura.
Ndege ya WesJet iliwasili Toronto ikitokea Cancun, Mexico na ilikuwa tayari imesimama wakati ajali hiyo ilitokea.
Huduma za dharura zilichukuliwa kwa haraka na abiria wakaondolewa.


No comments:
Post a Comment