TANGAZO


Tuesday, December 19, 2017

Marekani yailaumu Korea Kaskazini kwa kirusi cha WannaCry

White House Homeland Security adviser Tom Bossert speaks to reporters about the global WannaCry "ransomware" cyber attack in May

Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionThomas Bossert ambaye ni msadizi wa Rais Donald Trump, aliyesama haya kupitia jarida la Wall Street Journal.
Utawala nchini Marekani unasema kuwa Korea Kaskazini ilihusika moja kwa moja na kirusi cha wannaCry kilichoadhiri hospitali, biashara na mabenki kote duniani mapema mwaka huu.
Kirusi hicho kilidaiwa kuvamia zaidi ya kampuni 300,000 kwenye mataifa 150 na kusababisha hasara ya mabilioni ya dola.
Thomas Bossert ambaye ni msadizi wa Rais Donald Trump, aliyasema haya kupitia jarida la Wall Street Journal.
Hii ndiyo mara ya kwanza Marekani imeilaumu Korea Kaskazini kwa kirusi hicho.
A programmer shows a sample of the WannaCry locked encryption page on a laptopHaki miliki ya pichaEPA
Image captionKompyuta zinazotumia Windows zilivamiwa na kirusi hicho na kufungwa ambapo watumiaji walitakiwa kulipa ili kuweza kupata data zao
Bw. Bossert anayemshauri Trump katika masuala ya usalama wa ndani wa nchi alisema kuwa madai hayo ni kutokana na ushahidi uliopo.
Serikali ya Uingereza na kampuni ya kompyuta ya Microsof waliilaumu Korea Kaskazini kwa kirusi hicho.
Mwezi Mei kompyuta zinazotumia Windows zilivamiwa na kirusi hicho na kufungwa ambapo watumiaji walitakiwa kulipa ili kuweza kupata data zao.
Kim Jong-Un in an image released by North Korean news agency on December 12, speaking into microphone at a munitions conferenceHaki miliki ya pichaKCNA/AFP
Image captionKorea Kaskazini haijajibu madai hayo

No comments:

Post a Comment