TANGAZO


Sunday, November 26, 2017

Maandamano Islamabad : Jeshi la Pakistan lasema liko tayari kusaidia

Watu 200 walijeruhiwa katika mapigano ya Jumamosi

Haki miliki ya pichaEPA
Image captionWatu 200 walijeruhiwa katika mapigano ya Jumamosi
Jeshi la Pakistan linasema "liko tayari" kuisaidia serikali kuwatawanya waandamanaji wenye itikadi kali za kiislamu walioifunga barabara kuu wa Islamabad.
Serikali ililiomba jeshi liisaidie kurudisha utulivu baada ya polisi kushindwa kuwatawanya waandamanaji Jumamosi.
Hatahivyo taarifa ya jeshi inaonekana kuishutumu serikali kwa namna ilivyoshughulikia hali, ikieleza kuwa maafisa wa polisi hawakutumiwa vizuri.
Inaaminika kuwa takriban watu 6 wameuawa.
Wengine takriban 200 wamejeruhiwa.
Jeshi limeomba ufafanuzi zaidi kabla ya kuagiza kutumwa kwa wanajeshi.
Wengi ya waliojeruhiwa ni maafisa wa usalamaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionWengi ya waliojeruhiwa ni maafisa wa usalama
Waandamanaji wamefunga barabara kwa wiki kadhaa wakitaka waziri wa sheria Zahid Hamid, afutwe kwa kazi kwa makosa ya kukufuru.
Maandamano yamesambaa hadi katika miji mingine ukiwemo Lahore na bandari ya kusini Karachi.
Siku ya Jumamosi, serikali ilifunga kwa muda vituo vya kibinfasi vya habari na kufunga baadhi ya mitandao ya kijamii ukiwemo Facebook, Twitter na Instagram - kutokana na wasiwasi kwamba matangazo ya moja kwa moja ya hatua ya polisi huenda yakachochea hisia kali za kidini.
Vyombo vya habari nchini vinasema vimesalia kufungwa siku ya Jumapili.

No comments:

Post a Comment