TANGAZO


Sunday, November 26, 2017

Chui milia auawa kwa kuzurura mjini Paris

Tiger - archive pic

Image captionHaijulikani alitoroka vipi kutoka kwenye sarakasi
Chui milia alitoroka sarakasi na kuzunguka mjini Paris kuisni mwa jengo la Eiffel kabla ya maafisa wanaomshughulikia kumpiga risasi na kumuua.
Polisi walituma ujumbe kwenye twitter kwamba kulikuwa na chui milia anayezurura lakini 'hatari imeondolewa'.
Hakuna aliyejeruhiwa na chui milia huyo mwenye uzito wa kilo 200, kwa mujibu wa taarifa kutoka eneo hilo.
Usafiri wa treni ulisitishwa katika eneo hilo. Wakaazi wakaita maafisa wa huduma za dharura walipomuona mnyama huyo akikimbia mwendo wa saa kumi na mbili jioni kwa saa za huko.
"Alikuwa mkubwa," mwanamume mmoja kwa jina Ralph ameuambia mtandao wa Le Parisien. "Tulisikia milio miwili au mitatu ya risasi na tukaona polisi wakielekea kwenye barabara ya chini."
Aliuawa kichochoroni, msemaji mmoja wa zima moto alieleza.
Mmiliki wake aliyemuua chui milia huyo anazuiwa na polisi shirika la habari la AFP linaripoti kwa kunukuu duru na kuongeza kuwa polisi wameanzisha uchunguzi.
Chui milia huyo alipigwa risasi na mmiliki wakeHaki miliki ya pichaAFP
Image captionChui milia huyo alipigwa risasi na mmiliki wake

No comments:

Post a Comment