TANGAZO


Monday, November 27, 2017

Bate Borisov walivyoshinda ligi dakika ya 96 Belarus

Bate Borisov

Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionBate Borisov walishinda taji la ligi mara ya 14 nchini Belarus
Bate Borisov walifanikiwa kushinda taji la ligi kwa mara ya 12 mtawalia nchini Belarus kwa njia ya kipekee - kwa kufunga bao dakika ya 96.
Dinamo Minsk, ambao walikuwa wanashindania taji hilo walikuwa wameshinda mechi yao 4-1 na walikuwa na kila matumaini ya kutwaa ubingwa kwani Bate Borisov walikuwa nyuma mechi yao.
Lakini bahati yao haikusimama. Mirko Ivanic alifunga bao la kusawazisha dakika ya 96 na kufanya mambo kuwa 3-3 wakiwa ugenini dhidi ya Gorodeya.
Sare yao iliwasaidia kushinda ligi kwani walikuwa wamewazidi nguvu Dinamo klabu hizo zilipokutana.
Klabu zote mbili zilimaliza ligi zikiwa na alama 68.
Tofauti ya mabao ya Bate ni +42 nao Dinamo walikuwa na +31.
Dinamo Minsk mara ya mwisho walishinda ligi 2004.
Bate BorisovHaki miliki ya pichaBATE BORISOV
Shakhtyor Soligorsk ilikuwa klabu ya mwisho, kando na Bate, kushinda taji hilo, mwaka 2005.
Dinamo walikuwa wameshinda msimu uliotangulioa.
Bate walikuwa nyuma 3-1 mechi yao wakati mmoja kabla ya kufungiwa penalti na Vitali Rodionov mechi ikiwa imesalia na dakika 12 muda wa kawaida.
Kwa sasa wanashika mkia Kundi H katika Europa League na wanahitaji kulaza Arsenal tarehe 7 Desemba ndipo wawe na matumaini ya kusonga kutoka hatua ya makundi.

No comments:

Post a Comment