TANGAZO


Monday, October 2, 2017

WAJUMBE MKUTANO MKUU WA 45 WA CHAMA CHA WAUGUZI TANZANIA (TANNA) SAFARINI LINDI


Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Wauguzi Tanzania  (TANNA)  kutoka sehemu mbalimbali wakiungana na wajumbe wenzao pamoja na viongozi wa Tanna Mkoa wa Lindi jana katika kufanya maandalizi ya Mkutano Mkutano Mkuu  wa 45 unao tarajiwa kufanyika Oktoba 4-6 Kitaifa  ambapo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mh. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa.(PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)

Mwenyekiti wa Chama Cha Wauguzi Tanzania (TANNA) Mkoa wa Lindi, Patrick Achimpota (kulia) mwenyeshati la kitenge akisalimiana na mjumbe wa Kamati kuu ya Chama hicho kutoka Arusha, Hosea Naman mara alipofika Mkoani humo kwa niaba ya Mkutano Mkuu wa Chama hicho.


Wajumbe wa Chama Cha Wauguzi (TANNA) wakiwa katika safari kuelekea Mkoa wa Lindi katika Mkutano Mkuu wa Chama hicho  unao tarajiwa kufanyika Oktoba 4-6 Kitaifa ambapo unatarajiwa kufunguliwa na Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa.
 


Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Mkoa Lindi, Damasiana Msala (kulia)  akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Wauguzi (TANNA) mara walipowasili katika mkoa huo jana
Makamu wa Rais wa Chama hicho, Ibrahim Mgoo (wa katikati) akisalimia wajumbe mara baada ya kuwasili katika Mkoa huo jana, kulia ni Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Mkoa Lindi, Damasiana Msala na kushoto ni Katibu Mkuu wa Chama hicho, Sebastian Luziga.

Katibu Mkuu wa Chama hicho, Sebastian Luziga (kushoto) akisalimia wajumbe mara walipowasili jana Mkoani Lindi, kulia ni  Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Mkoa Lindi, Damasiana Msala na Makamu wa Rais wa Chama hicho, Ibrahim Mgoo.
Mkurugenzi wa Maendeleo wa Chama cha Wauguzi (TANNA), Charles Soloka (kushoto) atowa taarifa ya  majumuoisho ya maandalizi ya Mkutano huo jana.

No comments:

Post a Comment