Utangulizi
Mheshimiwa Rais,
KAMA ambavyo Watanzania watakumbuka tarehe 10 Aprili 2017, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt John Pombe Joseph Magufuli aliteua Kamati Maalum ya Kuchunguza Masuala ya Kisheria na Kiuchumi Kuhusiana na Mchanga wenye Madini unaosafirishwa nje ya nchi yakiwemo makontena 277 yaliyozuiliwa na Serikali katika Bandari ya Dar es Salaam.
Wajumbe wa Kamati ni:
1. Prof. Nehemiah Eliakim Osoro (Mwenyekiti)
2. Prof. Longinus Kyaruzi Rutasitara 3. Dr. Oswald Joseph Mashindano
4 Bw. Gabriel Pascal Malata
5. Bw. Casmir Sumba Kyuki
6. Bi. Butamo Kasuka Philip
7. Bw. Usaje Benard Asubisye
8. Bw. Andrew Wilson Massawe
2. Prof. Longinus Kyaruzi Rutasitara 3. Dr. Oswald Joseph Mashindano
4 Bw. Gabriel Pascal Malata
5. Bw. Casmir Sumba Kyuki
6. Bi. Butamo Kasuka Philip
7. Bw. Usaje Benard Asubisye
8. Bw. Andrew Wilson Massawe
Mheshimiwa Rais, katika kutekeleza uchunguzi huo, Kamati Maalum iliongozwa na Hadidu za Rejea zifuatazo:
1. Kufanya tathmini ya mchakato mzima wa usafirishaji wa makinikia na kujiridhisha iwapo utaratibu huo unafanyika kwa mujibu wa Mikataba iliyoingiwa baina ya Serikali na Makampuni ya uchimbaji wa madini “Mining Development Agreements” (MDAs) na “Special Mining Licence” (SPL) na kwamba taratibu hizo zinafuatwa kikamilifu. Pamoja na masuala mengine ambayo Kamati itaona ni muhimu kuyafuatilia, Kamati ijiridhishe kuhusu mrejesho wa taarifa za uchenjuaji wa makinikia kutoka nje ya nchi kwa mamlaka za Serikali.
2. Kupitia Mikataba husika na kushauri endapo inazingatia kikamilifu maslahi ya nchi ama inahitaji kuboreshwa. Maeneo yenye mapungufu na mapendekezo ya maboresho yabainishwe wazi.
3. Kufanya tathmini ya mfumo mzima wa udhibiti kuhusu biashara ya makinikia kutoka kuchimbwa, kusafirishwa, kuyeyushwa na kuuzwa kwa madini yanayopatikana katika makinikia hayo kwa lengo la kubainisha ufanisi wa mfumo huo katika kuzuia upotevu wa mapato ya Serikali yanayotokana na usafirishaji wa makinikia nje ya nchi.
4. Kupitia taarifa ya Kamati ya Wataalam ya kuchunguza kiwango na aina ya madini yaliyomo kwenye makontena yenye makinikia ya dhahabu yaliyokusudiwa kusafirishwa nje ya nchi, iliyoteuliwa tarehe 29 Machi 2017, hususan, kuhusu aina, kiasi, viwango vya ubora na thamani za madini yaliyomo kwenye makinikia hayo na kubainisha kama Serikali inapata mapato stahiki ya kikodi kutokana na biashara hiyo kwa mujibu wa mikataba na sheria za nchi.
5. Kubaini idadi ya makontena yenye makinikia yaliyosafirishwa kutoka katika migodi ya dhahabu kuanzia mwaka 1998 hadi sasa; na kwa kuzingatia taarifa ya Kamati ya Wataalam iliyotajwa katika aya ya 4, Kamati ifanye makadirio ya kiasi cha mapato ambacho Serikali ingestahili kupata na kulinganisha na kiasi halisi cha mapato kilichopatikana katika kipindi hicho.
6. Kubaini na kujiridhisha kama kuna sababu zozote za msingi za kiuchumi na kiufundi zinazokwamisha uanzishwaji wa kiwanda cha kuyeyusha makinikia nchini na kuishauri Serikali ipasavyo. Taarifa hiyo ibainishe:
i. Nini kinahitajika ili teknolojia ya kuchenjua mchanga kuwepo hapa nchini;
ii. Ni gharama kiasi gani zinahitajika ili kuanza uchenjuaji wa makininkia hapa nchini;
iii. Inachukua muda gani kukamilisha ujenzi wa mtambo husika hadi kuanza kufanya kazi;
iv. Nchi ina uwezo au mapungufu gani katika kulitekeleza hilo hasa katika upande wa wataalam na uwekezaji.
v. Aidha, Kamati ibainishe na kujiridhisha kuhusu hatua zilizochukuliwa na kampuni za uchimbaji dhahabu nchini katika kutekeleza sera na sheria za nchi kuhusu uanzishwaji wa kiwanda cha kuchenjua makinikia.
7. Kuchunguza na kulinganisha taarifa za uchunguzi wa kimaabara wa makinikia zinazotolewa na kampuni ya SGS Tanzania Superintendence Company LTD
(maabara binafsi inayopima sampuli za makinikia ya kampuni za madini) na Wakala wa Uchungzi wa Madini Tanzania (Tanzania Mineral Audit Agency –TMAA). Aidha, Kamati ibainishe ushiriki na majukumu ya kampuni nyingine ikiwamo SGS kuhusu makinikia.
8. Kubainisha uwepo wa mikataba na maudhui yake kati ya kampuni za uchimbaji madini ya dhahabu Tanzania na kampuni za uchenjuaji wa makinikia yanoyosafirishwa ili kijiridhisha kuhusu uhalali wa biashara hiyo na kama kodi na tozo mbalimbali za Serikali zililipwa ipasavyo.
9. Kuangalia mambo mengine yoyote yenye uhusiano na mchakato mzima wa usafirishaji wa makinikia, na kutoa mapendekezo ya kuboresha taratibu husika kwa siku zijazo kwa maslahi ya nchi.
10. Kufanya kazi kwa karibu na wataalamu katika Sekta ya Madini waliobobea katika taaluma zao wakiwemo Wanajiolojia, Wahandisi wa uchenjuaji (Metallurgists), Wakemia (Chemists), Wataalamu wa masuala ya Fedha na Wachumi pamoja na wataalam wa masuala ya sheria na kodi, kadri itakavyoona inahitajika.
11. Endapo itafaa, kuongeza Hadidu za Rejea katika kuboresha utekelezaji wa majukumu yake. Aidha, Kamati itakuwa na mamlaka ya kumwita mtu yeyote au kuwasiliana na ofisi yoyote ya Serikali (kupitia Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi) kwa lengo la kupata taarifa muhimu zinazohitajika.
Utekelezaji wa Majukumu
Mheshimiwa Rais,
Katika kutekeleza uchunguzi huo, Kamati ilifanya mambo yafuatayo:
1. Kuandaa Mpango Kazi, kukusanya na kupitia mikataba, sheria, sera za madini na kodi, hususan mikataba ya utafiti, uchimbaji, usafirishaji na uuzaji wa madini na makinikia, kuchambua na kuhakiki mfumo mzima wa udhibiti wa biashara ya makinikia, na taarifa kupokea taarifa kutoka mamlaka za Serikali nchini na nje ya nchini kuhusiana na uchenjuaji wa makinikia.
2. Kutembelea na kupata taarifa kutoka sehemu na taasisi zifuatazo:
i. Migodi ya Bulyanhulu Gold Mines Ltd (Acacia Gold Mining Plc), Pangea Gold Mine Ltd (Acacia Gold Mining Plc), North Mara Gold Mine Ltd (Acacia Gold Mining Plc), Geita Gold Mine Ltd
(AngloGold Ashanti Ltd); ii. Mamlaka ya Bandari Tanzania kwa lengo la kuona na kupima uzito wa makontena 277 yenye makinikia yaliyozuiliwa na Serikali; na
iii. Mamlaka ya Mapato Tanzania, Ofisi Kuu ya Takwimu, Wizara ya Nishati na Madini, Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania(TMAA), Shirika la Madini Tanzania(STAMICO) na Ofisi ya Msajili wa Makampuni (BRELA), Mamlaka ya Masoko ya Hisa na Mitaji (CMSA);
3. Kuwaita na kufanya mahojiano na:
i. Watendaji wakuu Serikalini na watumishi wa taasisi za Serikali na binafsi; na
ii. Watu binafsi wenye ujuzi na uzoefu katika sekta ya madini, usafirishaji wa mizigo na wakala wa meli.
4. Kupata taarifa na kujifunza kutoka kwenye nchi nyingine zilizofanikiwa katika biashara ya madini na uchenjuaji wa makinikia.
5. Kukusanya na kufanya uchambuzi wa takwimu za makontena ya makinikia yaliyosafirishwa nje ya nchi na takwimu za kiuchumi na kodi ili kubaini kodi halisi iliyolipwa na kodi ambayo ilipaswa kukusanywa kutokana na biashara ya uuzaji wa makininkia nje ya nchi kuanzia mwaka 1998 hadi mwaka 2017.
6. Kufanya uchambuzi kuhusu uwezekano wa ujenzi wa kiwanda cha uchenjuaji wa makinikia nchini.
7. Kufanya uchambuzi wa taarifa za kimaabara za makinikia zilizotolewa na kampuni ya maabara binafsi inayopima sampuli za makinikia ya madini (SGS), Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA) na Kamati Maalum Namba 1.
Matokeo ya Uchunguzi
Mheshimiwa Rais
1. Uhalali wa Kisheria wa Kampuni ya Acacia Mining Plc nchini Tanzania.
Kamati imebaini na kuthibitisha kwa mujibu wa nyaraka na maelezo kutoka ofisi ya Msajili wa Makampuni (BRELA) kuwa kampuniya Acacia Mining Plc haikusajiliwa (incorporation) nchini Tanzania na wala haina hati ya utambuzi (certificate of compliance) kwa mujibu wa Sheria ya Makampuni, Sura ya 212.
Kamati pia imebaini kuwa kampuni ya Acacia Mining Plc, ambayo inajinasibisha kuwa mmiliki wa makampuni ya Bulyanhulu Gold Mines Ltd, North Mara Gold Mine Ltd na Pangea Minerals Ltd, haikuwahi kuwasilisha nyaraka wala taarifa yoyote kuonesha kuwa kampuni hiyo ni mmiliki wa makampuni hayo wala kuwa na hisa katika makampuni hayo. Kwa kuwa Acacia Mining Plc haina usajili wala utambuzi wa kisheria nchini Tanzania, haina sifa ya kupata leseni, kuchimba wala kufanya biashara ya madini nchini Tanzania. Hivyo basi, Kamati imebaini kuwa Acacia Mining Plc, inafanya biashara ya madini hapa nchini kinyume cha sheria za nchi.
2. Biashara ya Uuzaji na Usafirishaji wa Makinikia Nje ya Nchi
Mheshimiwa Rais,
Kamati ilibaini kuwa makampuni ya Bulyanhulu Gold Mines Ltd na Pangea Minerals Ltd ndizo wazalishaji na wauzaji wa makinikia nje ya nchi. Kwa mujibu wa mikataba ya mauzo ya makinikia baina ya makampuni hayo na wafanyabiashara kutoka nje ya nchi, makinikia husafirishwa kutoka Tanzania yakiwa yameshauzwa na hupelekwa nje ya nchi kwa madai ya kwenda kuchenjuliwa kupitia Bandari za Dar es Salaam na Tanga. Makinikia hayo hupelekwa nchi za China, Japani na Ujerumani, yakiwa kwenye makontena yenye urefu wa futi 20 na wastani wa tani 20 kila moja.
Wafanya biashara wa makinikia ni makampuni yaitwayo Aurubis AG na Aurubis Bulgaria ADM, Mark Rich Co. Investment AG na Pan Pacific Copper Co. Limited kutoka nchi za Ujerumani, Uswisi na Australia. Mauzo hayo ya makininkia hufanywa kwa mujibu wa mikataba ya uchimbaji wa madini kati ya Serikali na Makampuni ya uchimbaji madini (Mining Development Agreements-MDAs). Kutokana na taarifa za kiuchunguzi (forensic investigation) kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mauzo ya makininkia hufanyika kupitia Ofisi ya Uhasibu (Treasury Department) ya makampuni hayo iliyopo Afrika ya Kusini.
3. Utaratibu wa Uuzaji Makinikia Nje ya Nchi
Mheshimiwa Rais,
Kamati imebaini kwamba kifungu cha 51 cha Sheria ya Madini kinaruhusu mwenye leseni ya uchimbaji wa madini kufanya biashara ya madini, ikiwa ni pamoja na kuuza nje ya nchi. Kifungu hicho kinamtaka mwenye leseni ya uchimbaji kupata kibali cha kusafirisha madini kutoka kwa Afisa Mwenye Mamlaka atayethibitisha kwamba mrahaba stahiki umelipwa kwa Serikali. Mbali ya kupata kibali kinachoonesha malipo ya mrahaba hakuna utaratibu mwingine maalum katika biashara ya uuzaji na usafirishaji wa makinikia nje ya nchi. Aidha, kisheria makampuni ya madini yanapaswa kutoa taarifa sahihi kwa Serikali kuhusu aina, kiasi na thamani ya madini yaliyomo ili kuiwezesha Serikali kukokotoa na kutoza mrahaba stahiki.
Mheshimiwa Rais,
Kwa kuzingatia nyaraka na taarifa mbalimbali za kiuchunguzi, Kamati imeridhika kuwa baadhi ya watumishi wa Serikali, watumishi na wamiliki wa makampuni ya madini, makampuni ya usafirishaji na upimaji wa madini na makampuni yenyewe yametenda makosa mbalimbali ya kijinai yakiwemo ukwepaji wa kodi, kutoa taarifa za uwongo, kujipatia mali kwa njia ya udanganyifu, uhujumu uchumi na kulisababishia taifa hasara kinyume cha:
i. vifungu vya 18,114 na 115 vya Sheria ya Madini,
2010 ii. vifungu vya 101 na 106 vya sheria ya kodi ya mapato, 2004
iii. vifungu vya 79 na 82 vya Sheria Usimamizi wa kodi, 2015
iv. kifungu cha 24 cha Sheria ya Uwazi na uwajibikaji katika sekta ya Madini Tanzania, 2015
v. Kifungu cha 27 cha Sheria ya Makosa ya Uhujumu
Uchumi sura ya 200, na vi. Kifungu cha 203 cha Sheria ya Usimamizi wa Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki,2004
Kwa kuzingatia nyaraka na taarifa mbali mbali za kiuchunguzi Kamati pia imeridhika kuwa baadhi ya watumishi wa Serikali, watumishi na wamiliki wa makampuni ya madini, makampuni ya usafirishaji na upimaji wa madini na makampuni yenyewe wamelitia aibu Taifa kwa kutenda makosa mbali mbali yakiwemo, ukwepaji wa kodi, kutoa taarifa za uwongo, kujipatia mali kwa njia ya udanganyifu, uhujumu uchumi na kulisababishia taifa hasara.
Mheshimiwa Rais,
Kamati pia imebaini kwamba, katika kufanya biashara ya makiniki


No comments:
Post a Comment