TANGAZO


Tuesday, February 7, 2017

BARAZA LA USHINDANI LAJIDHATITI KUWAHUDUMIA WANANCHI

Mshauri wa Sheria wa Baraza la Ushindani Tanzania (FCT) Bw. Ikunda Mkenda akiwaeleza waandishi wa habari (hawapo pichani)Leo Jijini Dar es salaam kuhusu mikakati ya Baraza hilo katika kushughulikia rufani za mashauri yanayowasilishwa kutokana na maamuzi ya Tume ya Ushindani(FCC) pamoja na Mamalaka za udhibiti kama EWURA,TCAA,SUMATRA na TCRA. kulia ni Mchumi Mwandamizi wa Baraza hilo Bw. Nonge Ally.(Picha zotr na Frank Mvungi-Maelezo)
Mchumi Mwandamizi wa Baraza la Ushindani Tanzania (FCT)  Bw. Nonge Ally akifafanua kwa waandishi wa Habari leo Jijini Dar es salaam kuhusu huduma zinazotolewa na Baraza hilo katika kuhakikisha kuwa kuna ushindani wenye tija katika soko. Mshauri wa Sheria wa Baraza la Ushindani Tanzania (FCT) Bw. Ikunda Mkenda.
Mshauri wa Sheria wa Baraza la Ushindani Tanzania (FCT) Bw. Ikunda Mkenda akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) leo Jijini Dar es Salaam.  
Baadhi ya waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano wa Baraza la Ushindani Tanzania (FCT) leo Jijini Dar es Salaam.


Frank Mvungi-Maelezo
BARAZA la ushindani Tanzania (FCT) lapokea na kushughulikia mashauri 139 kati 164 yaliyowasilishwa kutokana na maamuzi ya Tume ya Ushindani pamoja na Mamlaka za Udhibiti ili kuweka mazingira ya usawa katika soko nchini.

Kauli hiyo imetolewa  na Mshauri wa Sheria wa Baraza hilo Bw. Kunda Mkenda wakati wa mkutano na waandishi  habari Leo Jijini Dar es Salaam.

Akifafanua suala hilo Mkenda amesema kuwa dhamira ya Baraza hilo ni kuhakikisha kuwa kunakuwa na ushindani wenye tija kwenye soko.

Akizungumzia majukumu ya Baraza hilo Mkenda alisema kuwa Baraza hilo linaweza kubadilisha uamuzi wa Tume ya ushindani au Mamlaka ya udhibiti  ili kuweka mazingira ya usawa katika utoaji wa huduma katika soko.

“Jukumu kubwa ni kukuza na kulinda ushindani wa haki na kumlinda mlaji dhidi ya matokeo ya ukiritimba na tabia potofu katika soko ili kuepusha athari katika  uchumi” Alisisitiza Mkenda.

Pia, aliongoza kuwa Baraza hilo linaweza kutoa adhabu, faini, amri, tamko au kuamuru kulipwa fidia kutokana na hasara anayokuwa amepata mlalamikaji au muwasilisihaji wa rufani katika Baraza.

Aidha, Mchumi Mwandamizi wa Baraza hilo Bw. Nonge Aly liongeza kuwa wananchi wanalo jukumu kubwa la  kutumia huduma zinazotolewa na Baraza hilo.


Baraza la Ushindani ni Chombo kilichoanzishwa na serikali chini ya kifungu cha 83 (1) cha Sheria ya ushindani namba 8 ya mwaka 2003.

No comments:

Post a Comment