Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC) Jaji mstaafu Damian Lubuva akizungumza na wajumbe wa kikao cha
Menejimenti ya tume hiyo (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC Bwana Kailima Ramadhani. (Picha na Christina Njovu, NEC)
MWENYEKITI wa Tume ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC) JajiMstaafu Damian Lubuvaamewasihi viongozi na
wafanyakazi wa tume hiyo kuzingatia nidhamu ya kazi ili kuletaufanisikatika
kutekeleza majukumu yao.
MwenyekitiLubuvaalitoanasaha
hizo katika Kikao cha Utawala kinachoongozwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi ambacho
hufanyika kila wiki kwa ajili ya kuimarisha utendaji kazi wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi.
Amesema kuwa kuzingatia
nidhamu katika kazi kutawasadia sio tu katika kutekeleza majukumu ya Tume
bali mahali popote ambapo mfanyakazi atapelekwa.
Aidha, Mwenyekiti Lubuva amewashukuru wakuu
hao wa Idara mbalimbali za Tume kutokana na ushirikiano waliouonesha wakati wa
Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
“Nakushukuru Mkurugenzi
wa Uchaguzi na timu unayoiongoza kwa jinsi mlivyofanya kazi kama timu na kuweza
kufanikisha Uchaguzi Mkuu uliopita najivunia kufanya kazi nanyi.”
Aidha, Lubuva alisisitiza nidhamu
ya kazi kwa viongozi na wafanyakazi kuwa ni muhimu sana katika kuleta ufanisi wa
kazi sio tu katika Tume bali mahali popote ambapo mfanyakazi atapelekwa.
Amewasihi wasipende kusukumwa
kufanya kazi na kwamba katika kutekeleza hilo mtu yeyote anatakiwa kujipanga na kuwa
tayari kufanya kazi ikiwa ni pamoja na kuwahi mahali pa kazi na kutimiza wajibu wake kwa
ufanisi.
Pia amesisitiza suala la
kuwa na uaminifu katika kazi ikiwa ni pamoja na masuala ya kijamii kwa ujumla
ambapo kutokana na hilo wananchi wataweza kuiamini taasisi nzima.
“Kama mlivyofanikisha uchaguzi uliopita fanyeni kazi kwa kujituma sio tu katika Uchaguzi
uliopita bali kwa kazi zilizopo na kazi zinazokuja ambapo kazi zilizopo mbele
yetu ni nyingi na kubwa.” Alisema, Mwenyekiti Jaji Lubuva na kufafanua kuwa.
“Kama mlivyofanikisha Uchaguzi
Mkuu uliopita pia fanyeni kazi kwa bidii kwa maandalizi ya chaguzi zijazo kwa ufanisi
na nidhamu.”
Aliwataka kuheshimiana kati yao kwa hiyo, itawawezesha
kufanya kazi kwa nidhamu kwa kufuata taratibu zilizowekwa ili kufanikisha shughuli
zilizopo mbele yao.
Akitoa neno la
shukrani, Mkuu wa Idara ya Huduma za Kisheria, Bwana Emmanuel
Kawishe amemshukuru Mwenyekiti Jaji Lubuva kwa namna alivyowaongoza na kufanikisha Uchaguzi Mkuu uliopita.
Bwana
Kawishe amemuahidi Mwenyekiti kwa niaba ya viongozi na wafanyakazi wenzake kuwa watatekeleza yale aliyowaasa na kumpongeza
kwa kufuata sheria wakati wa Uchaguzi mkuu uliyopita.
Kikao hicho ni
miongoni mwa vikao vinavyofanyika kila wiki kwa lengo la kuleta ufanisi katika
utendaji kazi katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

No comments:
Post a Comment