TANGAZO


Friday, November 11, 2016

BALOZI SEIF IDDI ALIVYOOMBOLEZA KIFO CHA SPIKA MSTAAFU SAMUEL SITTA

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akitia saini Kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Spika Mstaafu wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  ambae pia alikuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Marehemu Samuel Sita Nyumbani kwake Mtaa wa Masaki Jijini Dar es salaam. Kushoto  ni mkewe, Mama Asha Suleiman Iddi na mbele yake Balozi ni Picha ya Marehemu Mzee Samuel Sita.
Kikundi maalum cha Kwaya kilichotayarisha maalum kuimba nyimbo za maombolezo Nyumbani kwa Marehemui Mzee Samuel Sita wakati ibada za kuuaga mwili wake zikiendelea kwa Viongozi wa Kitaifa, Marafiki pamoja  na wana Familia nyumbani kwake Masaki Mjini Dar es Salaam. 
Baadhi ya wageni na wana familia waliohudhuria misa maalum ya kuuaga mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba ambae pia ni Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mzee Samuel Sitta. (Picha zote na Hassan Issa–OMPR – ZNZ)

No comments:

Post a Comment