Balozi wa Japani nchini Tanzania Bw. Masaharu YOSHIDA akizungumza katika afla fupi ya kuwaaga watumishi waliopata fursa ya kuhudhuria mafunzo ya Shahada ya Uzamili nchini Japani chini ya ufadhili wa Serikali ya Japani kupitia mpango wa ABE Initiative, iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japani nchini mapema leo
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Utumishi, Dkt. Laurean Ndumbaro akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi (12)waliopata fursa ya kuhudhuria mafunzo ya Shahada ya Uzamili nchini Japani chini ya ufadhili wa Serikali ya Japani kupitia mpango wa ABE Initiative awamu ya tatu (03), mara baada ya hafla fupi ya kuwaaga watumishi hao iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japani nchini mapema leo.
Watumishi (12) waliopata fursa ya kuhudhuria mafunzo ya Shahada ya Uzamili nchini Japani chini ya ufadhili wa Serikali ya Japani kupitia mpango wa ABE Initiative awamu ya tatu (waliosimama) wakijitambulisha mbele ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi, Dkt. Laurean Ndumbaro ( wa pili kulia mstari wa mbele) na Waandishi wa Habari (kushoto) wakati wa kipindi cha maswali na majibu mara baada ya hafla fupi ya kuwapongeza na kuwaaga watumishi hao iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japani nchini mapema leo.
Mwandishi wa habari wa gazeti la Dailynews Bi. Hilda Mhagama (wa kwanza kushoto) akiuliza swali kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Utumishi, Dkt. Laurean Ndumbaro( wa pili kulia mstari wa mbele) wakati wa kipindi cha maswali na majibu mara baada ya hafla fupi ya kuwapongeza na kuwaaga watumishi hao iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japani nchini mapema leo.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Utumishi, Dkt. Laurean Ndumbaro (wa pili kulia mstari wa mbele) akijibu swali aliloulizwa na Mwandishi wa habari wa gazeti la Dailynews Bi. Hilda Mhagama (wa kwanza kushoto) wakati wa kipindi cha maswali na majibu mara baada ya hafla fupi ya kuwapongeza na kuwaaga watumishi waliopata fursa ya kuhudhuria mafunzo ya Shahada ya Uzamili nchini Japani chini ya ufadhili wa Serikali ya Japani kupitia mpango wa ABE Initiative awamu ya tatu, iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japani nchini mapema leo.
MAHUSIANO yaliyodumu kwa
muda mrefu baina ya Serikali ya Tanzania na
Japani yamewezesha watanzania zaidi ya 1000
kupata mafunzo katika vyuo mbalimbali
nchini Japani kwa kipindi cha
miaka 8 ambayo yamesaidia kuwa na
rasilimaliwatu yenye tija katika maendeleo ya kiuchumi nchini Tanzania.
Hayo yalisemwa
na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menentimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro kwenye hafla fupi ya
kuwaaga watanzania 12 waliopata fursa ya mafunzo
ya Shahada ya Uzamili nchini Japani
kwa ufadhili Serikali ya
Japani kupitia Mpango
wa ABE initiative,
iliyofanyika leo nyumbani kwa balozi wa
Japani nchini Tanzania .
“ Kati ya mwaka 2008 hadi 2015 zaidi ya watanzania 1000 wamepata mafunzo katika vyuo mbalimbali nchini Japani
kupitia ufadhili wa Shirika la
kimataifa la Maendeleo la Japani ( JICA) na hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa
katika kuwajengea uwezo watumishi wa umma na watumishi walio katika
sekta binafsi” alisema Dkt. Laurean
Ndumbaro.
Dkt.
Ndumbaro alifafanua kuwa, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma kwa kushirikiana na Shirika la
Kimataifa la Maendelo la Japani limewawezesha vijana wengi wa kitanzania kupata
mafunzo ya shahada ya Uzamili kupitia Mpango wa ABE initiative,ambao
baada
ya kumaliza mafunzo , wanarudi nchini
Tanzania na kuanza kujenga ushirikiano
wa kibiashara kati ya Tanzania
na Japani na pia kuchangia
katika maendeleo ya sekta ya
viwanda nchini” alisisitiza Dkt. Ndumbaro.
“ Katika
awamu ya kwanza mwaka 2014
walienda vijana 29 na awamu ya pili ambayo ni mwaka 2015 walienda
vijana 32 kwa ajiri ya kupata mafunzo nchini Japani, ambapo mpaka sasa
idadi ya wanufaika wa mafunzo hayo imefikia 73” alifafanua Dkt. Ndumbaro.
Aidha Dkt. Ndumbaro aliwataka vijana waliopata fursa ya mafunzo hayo nchini
Japani kusoma kwa bidii na kutumia elimu na ujuzi watakaoupata kuleta
maendeleo ya kiuchumi nchini.
Alisema, ushirikiano baina ya Serikali ya Tanzania
na Japani umeanza tangu mwaka
1960 ambapo kwa mara ya kwanza Tanzania ilipata
fursa ya kupeleka watanzania nchini
Japani mwaka 1962 kwa ajili ya kupata mafunzo
katika vyuo mbali mbali nchini humo.
Kwa upande
wake Balozi wa Japani nchini Mhe. Masaharu Yoshida alisema, Japan
itaendelea kudumisha ushirikiano wa muda mrefu uliopo baina ya nchi hizo mbili
ili kila upande unufaike kupitia ushirikiano huo.
Naye Mwakilishi Mkazi Mwandamizi wa Shirika la Kimataifa
la Maendeleo la Japani nchini (JICA)
Bw. Toshie Nagase amesema, vijana 12 waliopata nafasi ya mafunzo
nchini Japani kupitia Mpango wa ABE initiative ni kati ya
52 walioomba nafasi hiyo, hivyo hawanabudi kuitumia fursa hiyo kujifunza kwa bidii kwa ajili ya manufaa ya nchi.
Mpango wa
ABE initiative wa
miaka 5
ulianzishwa nchini Japani mwaka 2013 na
Waziri Mkuu wa Japani Mhe. Shinzo ABE ambaye alitambua umuhimu wa
kusaidia uwezeshaji wa maendeleo endelevu ya kiuchumi barani Afrika, mpango huo
ulilenga kunufaisha vijana 1000 wa kiafrika.

No comments:
Post a Comment