TANGAZO


Monday, June 20, 2016

Thamani ya naira yashuka dhidi ya dola ya Marekani

Image copyrightGETTY
Nigeria imeruhusu thamani ya sarafu yake kuyumba katika hatua za kuzuia kuwepo ukosefu wa sarafu za kigeni. Kutokana na hatua hiyo thamani ya naria ilishuka mara moja kwa asilimia 23.
Muda mfupi baada ya kuanza kwa biashara leo Jumatatu, thamani ya naira ilikuwa ni naira 255 kwa dola moja ya Marekani.
Thamani ambayo ilikuwepo awali ilikuwa ni naira 197 kwa dola.
Wachanganuzi wanasema kuwa kushuka kwa bei ya mafuta, imesabasia thamani ya naira kushuka.
Bei ya naira katika masoko yasiyo halali ni 350 kwa dola moja ya Marekani.

No comments:

Post a Comment