Katibu mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Eng. Joseph Nyamhanga akifafanua jambo kuhusu mpango wa ujenzi wa kujenga fly overs katika jiji la Dar es Salaam kwa lengo la kupunguza msongamano wa magari katika jiji hilo kushoto ni muakilishi kutoka Kampuni ya Kimarekani ya Mabey Bridge Bw. Darren Keep na kulia ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa.
Msimamizi Mkuu wa Daraja la Nyerere Bw. Gerald Sondo akieleza jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kuhusu maendeleo ya Daraja pamoja na changamoto wanazozikabili, katika Ziara ya kushtukiza iliyofanya na Waziri huyo leo jijini Dar es Salaam.
Msimamizi Mkuu wa Daraja la Nyerere Bw. Gerald Sondo akieleza jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kuhusu maendeleo ya Daraja pamoja na changamoto wanazozikabili, katika Ziara ya kushtukiza iliyofanya na Waziri huyo leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akipata maelezo kutoka kwa Fundi mitambo Bw. Simon Dotto kuhusu maendeleo ya ukarabati wa mtambo wa kupima mafuta kutoka kwenye meli kabla ya kuingia kwenye matanki ambao uliharibika hivi karibu kutokana na mvua iliyoambatana na upepo mkali.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akipata maelezo kutoka kwa Fundi mitambo Bw. Simon Dotto kuhusu maendeleo ya ukarabati wa mtambo wa kupima mafuta kutoka kwenye meli kabla ya kuingia kwenye matanki ambao uliharibika hivi karibu kutokana na mvua iliyoambatana na upepo mkali.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa wahudumu wa kivuko cha Mv Magogoni kuhusu utaratibu wa ukatishaji tiketi katika kivuko hicho leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akipata maelezo na changamoto mbalimbali kutoka kwa abiria wanaotumia kivuko cha Mv Magogoni leo jijini Dar es Salaam.
Na Betrice Lyimo-MAELEZO
27/05/2016
Dar es Salaam
SERIKALI kwa kushirikiana na Kampuni ya Mabey Bridge ya nchini Uingereza wamejipanga kikamilifu kujenga barabara tatu za juu (Fly Overs) na barabara nne za watembea kwa lengo la kupunguza msongamano wa foleni jijini Dar es Salaam.
Profesa Mbarawa alisema kuwa barabara hizo zitajengwa hasa maeneo ambayo yana msongamano mkubwa wa magari ikiwa ni pamoja na eneo la barabara ya Mwenge.
“Serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha wananchi wanakuwa na miundombinu iliyobora hasa katika upande wa barabara za magari na barabara za waenda kwa miguu ili kuwarahisishia wananchi kuwahi kuwajibika katika maeneo yao ya kazi”.
Mbali na hayo, Waziri Mbarawa alifanya ziara ya kushtukiza katika Daraja la Nyerere lililopo maeneo ya Kigamboni kwa lengo la kutaka kujua maendeleo ya daraja hilo na kumtaka msimamizi wa daraja hilo kuandaa kadi maalumu au kitambulisho zitakazotumika kwa lengo la kupunguza msongamano wakati wa kulipia tozo.
vilevile Waziri aliwataka wananchi kuwa waangalifu na miundombinu ya daraja hilo na endapo kuna mtu atakaye bainika kuharibu atachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwa ni pamoja na kulipa faini za gharama ya juu.
“kuanzia sasa kunatakiwa kuwepo na faini kali kwa mtu yeyote atakaye haribu miundombinu ya daraja hili kwa lengo la kulifanya daraja lidumi kwa muda mrefu” alisisitiza Waziri Mbarawa.
Kwa upande wake Msimamizi Mkuu wa daraja la Nyerere, Gerald Sondo alisema wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya madereva wa daladala kushindwa kutumia daraja hilo na kudai kuwa tozo ni kubwa.
Vilevile Waziri huyo alifanya ziara katika eneo la ujenzi wa mtambo wa Mafuta kutoka kwenye meli kabla ya kuingia kwenye matanki (Flow Meter) kuona maendeleo ya ukarabati wa mtambo hio uliyoharibika hivi karibuni kutokana na mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali na kumtaka mkandarasi kuhakikisha eneo hilo linazungishiwa ukuta ili kuziba mitambo hiyo.

No comments:
Post a Comment