Bofya hapa kwa habari za karibuni zaidi
19:37 Kando na majimbo 12 ya Marekani, wapiga kura walio ng'ambo wanashiriki mchujo chama cha Democratic. Larry Sanders kakake mgombea wa Democratic Bernie Sanders, amepiga kura yake ya mchujo katika kituo cha Taasisi ya Marekani ya Rothermere, Oxford, UK nchini Uingereza.
Press Association
19:34 Upigaji kura utamalizika 1900 au 2000 EST (saa sita usiku au 01:00 GMT Jumatano) na matokeo yatatarajiwa kuanzia wakati huo.
Katika jimbo la Alaska, upigaji kura huendelea hadi saa sita usiku EST (05:00 GMT).
Getty
19:17 Upigaji kura kwa sasa unaendelea. Kuna majimbo 12 yanayochagua wagombea. Baada ya mchujo wa leo, jimbo la Colorado hufanya mkutano mkuu wa chama wa kugawa wajumbe.

19:15 Jumanne Kuu ilianzishwa 1988 kujaribu kutoa taswira kamili ya msimamo wa Wamarekani kuhusu wagombea na uwezo wao. Kwa maelezo muhimu kuhusu siku hii, soma: Mambo 5 muhimu kuhusu Jumanne Kuu
AFP y Reuters
19:10 (Saa za Afrika Mashariki) Hujambo! Karibu kwa habari za moja kwa moja kuhusu mchujo wa kuteua wagombea urais wa vyama vya Republican na Democratic katika majimbo 12 nchini Marekani.
Siku hii hufahamika sana kama Jumanne Kuu.

No comments:
Post a Comment