TANGAZO


Monday, February 22, 2016

Watanzania wapata fursa ya kujiunga na Elimu ya juu kwa Vyuo vya Nje

Bango linaloonyesha Mahali ambapo maonyesho ya Tanzania International Education ambapo wanafunzi wanapata fursa ya kudahili katika baadhi ya vyuo vikuu vya nje moja kwa moja kutoke jijini Dar es Salaam. Jumla ya vyuo 14 pamoja na taasisi moja ya kusaidia usarfiri kwa punguzo maalu kwa wanafunzi vinashiriki katika maonyesho hayo. 
Mshauri wa masuala ya Elimu kutoka Taasisi ya Aryan International Education Consultants ya nchini China Dkt. Safdar Khattak akitoa maelezo kuhusu namna ya kujiunga na Elimu ya Juu kwa wanafunzi wakitanzania waliotembela maonyesho ya Kimataifa ya Elimu “Tanzania Internation Education Fair 2016” yanayoendelea katika ukumbi wa British Council jijini Dar es Salaam. 
Mmoja wa wadau wa elimu aakijaza fomu ya kujiunga na Chuo Kikuu cha  BPP cha nchini Uingeraza alipotembelea maonyesho ya Tanzania Internation Education Fair 2016 jana jijini Dar es Salaam.Wanaomshuhudia ni Afisa Mtendajji Mkuu wa Taasisi ya WR Education Placement Consultant ya nchini Bw. Robert (kulia) na Mshauri wa Wanafunzi wa Education Placement Consultant Bi. Berinda. 
Mwakilishi wa Taasisi ya Sta Travel inayojihusisha na kusafirisha wanafunzi kwa punguzo ya gharama za usafiri Bw. Abbas Karrim akisikiliza maoni kutoka kwa baadhi ya wadau wa elimu waliotembelea meza yake katika maonyesho ya Tanzania Internation Education Fair 2016 yanayoendelea katika Ukumbi wa British Council jijini Dar es Salaam. 
 Mwakilishi kutoka Chuo Kikuu cha Eastern Medeterrenian cha nchini Uturuki akiwapa maelekezo wanafunzi wakitanzania waliotembelea meza yake katika maonyesho ya Tanzania Internation Education Fair 2016 yanayoendelea katika Ukumbi wa British Council jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi kutoka Chuo Kikuu cha Thompson cha nchini Canada Bi. Brenda Nicole akiwapa maelekezo wanafunzi wakitanzania waliotembelea meza yake katika maonyesho ya Tanzania Internation Education Fair 2016 yanayoendelea katika Ukumbi wa British Council jijini Dar es Salaam. 
Baadhi ya wanafunzi wakipitia machapisho ya vyuo mbalimbali  waliotembelea maonyesho ya Tanzania Internation Education Fair 2016 yanayoendelea katika Ukumbi wa British Council jijini Dar es Salaam. (Picha zote na Frank Shija)

No comments:

Post a Comment