TANGAZO


Wednesday, February 17, 2016

Cameroon yaishinda Misri voliboli

Image copyrightGuy Suffo CAVB
Katika Mechi ya Fainali ya mashindano ya voliboli ya wanawake afrika yaliyomalizika mjini Yaounde hapo jana, Cameroon imeishinda Misri kwa seti 3-2.
Kwa ushindi huo Cameroon italiwakilisha bara Afrika katika michezo ya Olimpiki mwezi Agosti mjini Rio Brazil.
Katika mechi ya kuwania mshindi wa tatu Kenya imewashinda Algeria seti 3-0 na kuzoa nishani ya shaba.
Nafasi ya tano imetwaliwa na Botswana, ikifuatiwa na Botswana na Uganda ikawa ya mwisho.

No comments:

Post a Comment