
Mtangazaji idhaa ya Kiswahili BBC London Maryam akimfanyia mahajiano nguli wa mitindo Bi. Asya Idarous Khamsin jijini London siku ya Ijumaa Februari 12, 2016 mahojiano maalum kwa ajili ya Lady in Red itakayofanyika leo Jumamosi Februari 13, 2016 mjini humo. Onyesho hilo litakalo washirikisha wasanii mbalimbali wakiongozwa na msanii wa Bongo Flava Rich Mavoko litakua ni sehemu ya kusherehekea siku ya wapendanao ambayo mwaka huu imeangukia siku ya Jumapili.
Kutoka kushoto ni msanii wa Bongo Flava Rich Mavoko, Mgalula Fundikila, Salim Kikeke na mama wa mitindo Asya Idarous Khamsini walipokua mjengoni idhaa ya Kiswahili BBC London.
Mtangazaji wa idhaa ya Kiswahili BBC London Sakuma Kssim akiwa katika picha ya pamoja na nguli wa mitindo Bi. Asya Idarous Khamsin wakati mwanamitindo huyo alipokua mjengoni huko kwa ajili ya kufanyiwa mahojiano.
Kutoka kushoto ni Saluma Kssim, Maryam, Aisha Yahya wakiwa katika picha ya pamoja mama nguli wa mitindo Asya Idarous Khamsini.





No comments:
Post a Comment