Bofya hapa kwa habari za karibuni zaidi
18:21 MECHI INAMALIZIKA Crystal Palace 0-3 Chelsea
Mabao yamefungwa na Oscar 29′, Willian 60′ na Diego Costa 66′.
18:20 Marouane Chamakh anashambulia, lakini anazimwa.
18:18 Palace wanashambulia, Courtois anaudaka mpira na kuurusha upesi kwa Willian anayeshambulia upande ule mwingine. Anajaribu kupenyeza mpira kwa Costa lakini kipa wa Palace yuko macho anauchukua.
18:17 Oscar anaondolewa uwanjani na nafasi yake anaingia Nemanja Matic
18:15 Diego Costa anajaribu kutikisa wavu kwa mpira mkali baada ya kupata mpira kutoka kwa Willian. Anatia nguvu zaidi na mpira unapaa juu ya wavu.
18:11 Jason Puncheon anachezewa vibaya na Fabregas. Anapewa frikiki.
18:09 Costa anaelekea kupata nafasi nzuri ya kufunga. Delaney anachomoka na kutoa mpira nje. Kona inapigwa na mpira unatoka nje.
18:08 Jonny Williams anaingizwa nafasi ya Lee Chung-yong upande wa Palace. Hajachezeshwa kwa kipindi cha miezi 16.
18:08 Diego Costa anachezewa vibaya na Scott Dann na kupata frikiki.
18:05 Zaha anashambulia, John Terry anatoa mpira nje na inakuwa kona. Haizai matunda.
17:58 Palace wanashambulia lakini Courtois anaudaka mpira.
17:58 Lee Chung-yong anajishindia frikiki baada ya kuchezewa vibaya na Mikel.
17:55 Marouane Chamakh anaingia nafasi ya Fraizer Campbell, Joe Ledley naye nafasi ya Mile Jedinak upande wa Palace.
17:54 BAOOO! Crystal palace 0-3 Chelsea
Diego Costa anafungia Chelsea la tatu.
Getty
17:52 Branislav Ivanovic anapata frikiki.
17:48 BAOOOO! Crystal Palace 0-2 Chelsea
Willian anatoa mpira mkali ambao unatua juu ndani ya wavu. Oscar alikuwa amechezewa vibaya lakini refa akaamua mchezo uendelee.
Reuters
17:46 Wilfried Zaha anachomoka, anabaki na kipa kati yake na lango lakinia anashindwa kumbwaga. Mambo baco Palace 0-1 Chelsea.
17:40 Chelsea wanapata frikiki baada ya Willian kuchezewa visivyo. Anaipiga. Zouma anaruka juu na kuufikia mpira kwa kichwa lakini anauelekeza juu ya wavu.
17:39 Palace wanashambulia kupita Zaha, lakini Mikel hapitiki.
17:38 Willian anatoa krosi ambayo inazimwa na mpira kutolewa nje. Inakuwa kona anaipiga na inatolewa nje. Anapiga tena lakini Palace wanauondoa hatarini.
17:36 Palace wanaanza kwa kushambulia, Jason Puncheon akitoa krosi kutoka kulia. Lakini mpira huo unadakwa na kipa Thibaut Courtois.
17:35 KIPINDI CHA PILI
17:18 WAKATI WA MAPUMZIKO
Crystal Palace 0 -1 Chelsea
17:17 Jason Puncheon (Crystal Palace) anashambulia lakini mpira wake unakosa goli. Palace wanajaribu tena lakini mpira unatua mikononi mwa Palace.
17:16 Pedro anafanya madhambi.
17:15 Pape Souaré anashinda frikiki.
17:10 Wilfried Zaha wa Palace anajishindia frikiki.
17:05 César Azpilicueta anapata mpira pahala pazuri, anashambulia lakini mpira wake unazimwa na kipa Wayne Hennessey.
17:02 Lee Chung-yong anashambulia lango la Chelsea, lakini mpira wake unapaa juu.
16:59 BAOOOO! Crystal Palace 0-1 Chelsea
Oscar anafungia Chelsea baada ya kupokea pasi nzuri kutoka kwa Diego Costa.
Reuters
16:55 Fraizer Campbell wa Palace anashambulia, lakini mpira wake unaelekea nje kulia.
Getty Images
16:50 Mechi inasimamishwa kwa muda baada ya Joel Ward wa Palace kuonekana kuumia. Baadaye inaendelea.
16:45 Mkwaju wa adhabu unapigwa. Mikel anatoa mpira nje na inakuwa kona ya Palace. Wanashindwa kufunga.
16:44 Pedro anaingia nafasi ya Eden Hazard anayeonekana kuumia.
16:43 Mkwaju wa adhabu dhidi ya Chelsea baada ya John Obi Mikel kucheza visivyo.
16:39 Damien Delaney wa Palace anaonyeshwa kadi ya manjano kwa kumchezea visivyo Diego Costa.
16:38 Chelsea wanapata kona baada ya Mile Jedinak kutoa mpira nje. Haizai matunda.
16:37 Palace waendelea kushambulia Chelsea, Wilfried Zaha akipoteza nafasi nzuri baada ya kupata mpira mzuri kutoka kwa James McArthur.
16:34 Mechi inacheleweshwa kidogo baada ya César Azpilicueta (Chelsea) kuonekana kuumia.
16:30 Crystal Palace 0-0 Chelsea
Palace wanaanza kwa kushambulia na wanapata kona baada ya Zouma kutupa mpira nje. Jason Puncheon anapiga kona hiyo lakini mwishowe mpira unatoka nje.
16:30 MECHI INAANZA
16:29 Hawa hapa ndio wachezaji wa timu zote mbili.
Chelsea

Crystal Palace

16:27 Fabregas na Diego Costa wamerejea kikosini. Costa alikuwa amesimamishwa mechi dhidi ya Manchester United ambayo iliisha 0-0.
Getty
16:25 Hujambo? Karibu kwa habari za moja kwa moja za Ligi Kuu ya England.
Leo Chelsea wako ugenini Selhurst Park kucheza dhidi ya Crystal Palace wakijaribu kujiinua chini ya meneja mpya Guus Hiddink.

No comments:
Post a Comment