TANGAZO


Sunday, December 27, 2015

China yapitishia sheria kali dhidi ya Ugaidi

Image copyrightBBC World Service
Image captionChina yapitishia sheria kali dhidi ya Ugaidi
Bunge la China limepitisha sheria ya kwanza katika taifa hilo inayolenga kukabiliana na tishio la ugaidi.
Sheria hiyo mpya inazishurutisha makampuni ya teknolojia ya mawasiliano kuipatia serikali taarifa nyeti kuhusiano na Mawasiliano.
Aidha kampuni hizo zitalazimika kutoa anuani za siri za watumiaji wake ikiwemo alama za kuficha mawasiliano.
Image copyrightAFP
Image captionSheria hiyo itaanza kutumika kuanzia Januari mosi mwakani.
Sheria hiyo itaanza kutumika kuanzia Januari mosi mwakani.
Serikali ya Washington hata hivyo imeonyesha wasiwasi wake juu ya sheria hiyo kuwa huenda ikawa na madhara kwa makampuni ya kibiashara ya kiteknolojia na kudidimiza uhuru wa kujieleza.
Serikali ya Uchina yenyewe imesema sheria hiyo ina ulazima hasa kwa wakati huu ambako matukio ya kigaidi hivi sasa yanazidi kuongezeka na kuhamia kwenye mitandao.

No comments:

Post a Comment