Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania, Mudhihir Mudhihir, akizungumza wakati alipokuwa akiufunga mkutano wa 3 wa Kimataifa wa Korosho, Dar es Salaam jana. Katikati ni Mtafiti Kiongozi wa Korosho nchini na Mratibu wa Kanda, Profesa Peter Masawe na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Dk. Hussein Mansour. (Picha na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Na
Lorietha Laurence-Maelezo
Bodi ya Korosho
Tanzania imeadhima kutoa asilimia 7 ya mapato yake sawa na shilingi bilioni
mbili kwa ajili ya kusaidia utafiti wa zao hilo
unaofanywa na kituo cha utafiti
cha Naliendele.
Akiongea wakati wa
kufunga kwa mkutano wa tatu wa kimataifa
uliowahusisha wadau kutoka nchi mbalimbli duniani ,Makamu Mwenyekiti wa
Bodi ya Korosho Tanzania Bw. Muhidhiri Muhidhiri amesema kuwa changamoto
kubwa wanayokabiliana nayo ni ukosefu wa fedha kwa ajili ya kuendeshea utafiti wa zao la korosho
unaofanywa na kituo cha Naliendele na hivyo wamejipanga kwa kuchangia kiasi cha mapoto ili
kufanikisha tafiti hizo.
Muhidhiri aliongeza kuwa licha ya changamoto za ukosefu
wa fedha wamepata fursa ya kujifunza mambo mbalimbali kupitia mkutano huo
ikiwemo maadhimio ya uzalishaji bora wa zao hilo, namna ya kutatua matatizo ya magonjwa
yanayoikumba korosho,dawa asilia zitakazosaidia katika kulinda mbegu, na njia
bora ya uzalishaji.
“Mkutano ulikuwa wa
kisayansi kwa kuwa umeangalia mambo ya
kiutafiti na teknolojia katika uzalishaji wa zao la korosho hivyo ninaamini baada ya hapa ni kuanza
utekelezaji wa yale tuliyoyajadili na kufanya vizuri zaidi ” alisema Muhidhiri.
Kwa upande wa Mtafiti
Mkuu wa Masuala ya korosho Prof.Peter
Masawe ameeleza kuwa mkutano huo wa wadau umewapa fursa ya kufahamu mambo
mazuri katika uboreshaji na uzalishaji wa zao la korosho katika kiwango kizuri
na kilicho bora.
Pia alibainisha kuwaTanzania
ndiyo nchi yenye mtafiti anayetegemewa katika masuala ya korosho na hivyo kupitia mkutano huo wadau wamepata fursa ya kufahamu mambo ya msingi kama vile mbegu bora
zinazozalishwa nchini ,mbegu fupi, mbegu
zinazostahimili ukame pamoja na kukopa
teknolojia ya uzalishaji.
“Mkutano huu umetoa
fursa kwa wadau kujua mambo muhimu kuhusu mbegu ukizingatia Tanzania ndiyo nchi
pekee barani Afrika inayozalisha mbegu bora hivyo natumai wajumbe wataenda kutendea
kazi yale yote waliyojifunza hapa kwetu na nasisi pia tutayafaniya kazi yale
tuliyoyapata kutoka kwao ” alisema Prof
Masawe.
Mkutano huo wa kimatifa
wa wadau wa Korosho umefanyika kwa mara ya pili nchini ambapo mara ya kwanza ilikuwa mwaka 1997 na
hivyo kuipa fursa nchi ya kujitangaza
kupitia sekta ya kitalii kwa
kuwahamasisha wadau waliohudhuria
mkutano huo kutembelea sehemu za vivutio ikiwemo Bagamoyo na Zanzibar.

No comments:
Post a Comment