TANGAZO


Monday, September 7, 2015

Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha Kanda ya Ziwa wapigwa msasa

Ofisa Vijana Kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni, na Michezo Bw. Godfrey Massawe akizungumza na vijana (hawapo pichani) wakati wa Mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha  kwa vijana wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa leo Jijini Mwanza. Mafunzo haya yamehusisha vijana kutoka Mkoa wa Simiyu, Mara, Kagera, Shinyanga na Mwanza. 
Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni, na Michezo Bw. James Kajugusi akisalimiana na vijana waliofika katika Mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha kwa vijana wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa leo Jijini Mwanza. 
Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni, na Michezo Bw. James Kajugusi akizungumza na vijana (hawapo pichani) wakati wa Mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha kwa vijana wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa leo Jijini Mwanza.
Mtaalamu wa masuala ya Vijana Bw. Benny Lugoe akitoa mada kuhusu viwango vya Stadi za Maisha kwa Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa leo Jijini Mwanza. 
Wawezeshaji wa Kitaifa wa masuala ya Stadi za Maisha kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa wakisikiliza kwa makini mada iliyokua ikiendelea wakati wa Mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa leo Jijini Mwanza. Kulia ni Mtaalamu wa masuala ya Vijana Bw. Robert Semkiwa. 
Wawezeshaji wa Kitaifa wa masuala ya Stadi za Maisha kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa wakijadiliana wakati wa mafunzo kwa vijana hao leo Jijini Mwanza. 
Mmoja wa Wawezeshaji wa Kitaifa wa masuala ya Stadi za Maisha Bw. Amos Owade akichangia mada wakati wa Mafunzo kwa Wawezeshaji wa Kitaifa leo Jijini Mwanza. Kushoto ni Bibi. Virginia Chacha 
Mwezeshaji wa Kitaifa wa masuala ya Stadi za Maisha Bibi. Stella Mbura akiwasilisha hoja mbalimbali walizojadili katika makundi wakati wa Mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa leo Jijini Mwanza. (Picha zote na: Genofeva Matemu – Maelezo, Mwanza)

No comments:

Post a Comment