TANGAZO


Wednesday, September 9, 2015

Wawezeshaji Kitaifa Kanda ya Ziwa watakiwa kuleta mitazamo chanya kwa vijana nchini

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga (kati) akizungumza na Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Dr. Faisal H. Issa (Kulia) alipotembelea Ofisini kwake kabla ya kufungua Mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha kanda ya ziwa jana jijini Mwanza. Kushoto ni Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi. (Picha zote na Genofeva Matemu – Maelezo, Mwanza) 
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga (kushoto) akimsikiliza  kijana ambaye ni Katibu wa Saccoss ya Vijana ya Bega kwa Bega Bi. Mabone James alipokutana nae katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza walipofika kujitambulisha kwa Mkuu wa Mkoa huyo kabla ya kufungua Mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha kanda ya ziwa jana jijini Mwanza. 
Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. James Kajugusi (kushoto) akifafanua jambo walipotembelea ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bw. Magesa S. Mulongo (kulia) kabla ya kufungua Mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha kanda ya ziwa jana jijini Mwanza. Wa pili kushoto ni Katibu Mkuu Wizara hiyo Bibi. Sihaba Nkinga, na wapili kulia ni Afisa Vijana Bibi. Diana Kasonga. 
Mwezeshaji wa kitaifa wa stadi za maisha Bibi. Octavina Kiwone (kulia) akimkaribisha mgeni rasmi katika Mafunzo ya Wawezeshaji kitaifa jana jijini Mwanza. Wapili kulia ni Mgeni rasmi katika Mafunzo hayo Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga, na kushoto ni Mkurugenzi wa Vijana Bw. James Kajugusi huku wa wapili kushoto ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Moses Pesha. 
Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. James Kajugusi (kushoto) akizungumza na Vijana (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa Mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha jana Jijini Mwanza. Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga, na katikati ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Moses Pesha. 
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga akifungua Mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha kanda ya ziwa jana jijini Mwanza. Kulia ni Mwezeshaji wa kitaifa wa stadi za maisha Bibi. Octavina Kiwone. 
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga (waliokaa katikati) katika picha ya pamoja na Wawezeshaji wa kitaifa wa stadi za maisha jana jijini Mwanza. Kushoto waliokaa ni Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi na wapili kulia waliokaa ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Moses Pesha. 
Wawezeshaji wa kitaifa wa Stadi za Maisha wakiangalia mbinu mbalimbali za uwezeshaji zilizowekwa ukutani wakati wa Mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha jna Jijini Mwanza. (Picha zote na Genofeva Matemu – Maelezo, Mwanza)

Na Genofeva Matemu - Maelezo, Mwanza
WAWEZESHAJI wa Kitaifa wa stadi za maisha wametakiwa kuwasaidia vijana kujitoa katika mitazamo hasi na kuleta mabadiliko chanya katika jamii  kwani vijana ni nguvu kazi ya Taifa letu.

Rai hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga alipokua akifungua Mafunzo ya siku nane kwa Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha jana Jijini Mwanza.

“Vijana wakijiimarisha katika shughuli za kijamii na kiuchumi wataepuka kuzungukwa na vihatarishi vya maisha kama vile HIV/AIDS, mimba zisizotarajiwa pamoja na madawa ya kulevya hivyo kujenga nchi kwa kutumia nguvu kazi ya vijana” alisema Bibi. Nkinga.

Aidha bibi.Nkinga amesema kuwa matarajio ya serikali ni kuona vijana wa kitanzania  wanajitambua kua wao ni nani, wanaenda wapi, na watafikaje kwa kujua uwezo na udhaifu binafsi walionao ili  waweze kupanga malengo waliyonayo na kuyatekeleza kulingana na fursa zilizopo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mafunzo hayo, Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara a Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. James Kajugusi amesema kuwa lengo la Mafunzo hayo kwa vijana ni kupata waelimishaji wa stadi za maisha wa kitaifa kwa kutumia vijana walio nje ya shule.

Aidha Bw. Kajugusi alisema kuwa Mafunzo haya yamelenga kupata waelimishaji wa kitaifa wa stadi za maisha watatu kutoka kila mkoa katika mikoa yote ya Tanzania bara ambao watawafikia waelimishaji rika wa kila mkoa ili kuweza kufikisha elimu waliyoipata kwa vijana wa rika mbalimbali katika Mikoa, Wilaya, kata, vijiji, vitongoji, mitaa, vijiweni na sehemu rasmi za shughuli za vijana.


Naye Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Dr. Faisal H. Issa amewashukuru waandaaji wa Mafunzo hayo kwa kuchagua kuanzisha mafunzo hayo kwa mikoa ya kanda ya Ziwa kwani ni jambo la neema kwa mikoa hiyo hivyo kuwataka Wawezeshaji wa Kitaifa Mikoa ya Kanda ya Ziwa kutumia nafasi waliyopewa kubadili fikra hasi za vijana katika mikoa ya kanda ya ziwa. 

No comments:

Post a Comment