TANGAZO


Saturday, September 12, 2015

Wanajeshi 19 wa UG waliuawa na Alshabaab

Image copyrightBBC World Service
Image captionRais Museveni
Rais wa Uganda Yoweri Museveni anasema kuwa wanajeshi wake 19 waliuawa kwenye shambulizi lililoendeshwa na wanamgambo wa Al shabaab nchini Somalia na wengine sita bado wakiwa hawajulikani waliko.
Museveni amewalaumu makamanda wa jeshi la Uganda kwa uzembe akisema kuwa ndiyo sababu iliosababisha kuuawa kwa wanajeshi hao wakati shambulizi lilipoendeshwa kwenye kambi ya jeshi la muungano wa Afrika eneo la Janale tarehe mosi mwezi huu.
Image captionWanajeshi wa AMISOM
Awali Uganda ilisema kuwa ni wanajeshi 12 waliouawa.
Alshabab wanasema kuwa wanazuilia wanajeshi wa Uganda kama wafungwa wa vita.

No comments:

Post a Comment