TANGAZO


Sunday, September 13, 2015

Wakimbizi 4000 waingia nchini Hungary

Image copyrightReuters
Image captionWakimbizi
Idadi kubwa zaidi ya wakimbizi wanaripotiwa kuingia nchini Hungary siku ya Jumamosi
Zaidi ya watu 4000 walitembea na kuvuka mpaka na serbia wakati ambapo utawala nchini Hungary unakamilisha mipango ya kufunga mpaka wake
Image copyrightReuters
Image captionPolisi wa Hungary
Hungary imeweka ua mwembamba na kutuma jeshi kusaidia polisi kufuata agizo lililotolewa na waziri mkuu wa nchi hiyo Victor Oban ambalo litaanza kutekelezwa siku ya jumanne.
Image copyrightReuters
Image captionWakimbizi walioingia Hungary
Awali Hungary ilimuita balozi wa Austria kutokana na mzozo uliopo kati ya nchi hizo baada ya Chansela wa Austria Werner Faymann kufananisha vitendo vya Hungary dhidi ya wahamiaji sawa na jinsi utawala wa Nazi nchini Ujerumani ulivyowatendea wayahudi.

No comments:

Post a Comment