TANGAZO


Wednesday, September 16, 2015

Wahamiaji wapata njia mpya Croatia

Image copyrightRENGIN ARSLAN
Image captionWahamiaji wa Syria
Kundi la kwanza la wahamiaji limewasili nchini Croatia ,ambayo ni njia mpya ya kuelekea mataifa ya Ulaya yaliopo kaskazini ,siku moja baada ya Hungary kufunga mpaka wake na Serbia.
Takriban wahamiaji 150 walivuka na kuingia katika mataifa ya muungano wa Ulaya kutoka Serbia.
Croatia inasema kuwa iko tayari kuwapokea moja kwa moja ama kuwaelekeza kule wanakotaka kwenda.
Wahamiaji wengi kutoka Syria wana matumaini ya kuelekea Ujerumani.
Image copyrightEPA
Image captionWahamiaji
Masharti mapya yaliowekwa katika mipaka pamoja na mzozo kuhusu kugawana maelfu ya wahamiaji hao kumezua tofauti kubwa miongoni mwa mataifa ya Ulaya.
Mamia ya wahamiaji waliokwama walingojea nje usiku kucha ama katika mahema karibu na mpakawa Serbia na Hungary.

No comments:

Post a Comment