TANGAZO


Wednesday, September 9, 2015

Rais Kikwete apokea hati za utambulisho wa Mabalozi 4 Ikulu jijini Dar leo

Balozi Mteule wa Uturuki nchini Yasemin Fraip akipigiwa wimbo wa Taifa wakati alipowasili Ikulu, Dar es Salaam leo, kuwasilisha hati za utambulisho kwa Rais Jakaya Kikwete.
Rais Jakaya Kikwete, akizungumza na Balozi Mteule wa Uswiss nchini, Florence Mattli, wakati alipofika Ikulu, kujitambulisha, Dar es Salaam leo.  
Balozi mpya wa Finland nchini Bw. Pekka Hukka akisanini kitabu cha wageni alipowasili Ikulu jijini Dar es Salaam kuwasilisha hati za utambulisho kwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo Septemba 9, 2015.
Balozi mpya wa Finland nchini Bw. Pekka Hukka akisoma salamu kabla ya kumkabidhi hati za utambulisho kwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam leo Septemba 9, 2015.
Balozi mpya wa Finland nchini Bw. Pekka Hukka akiwasilisha hati za utambulisho kwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam leo Septemba 9, 2015.
Balozi mpya wa Finland nchini Bw. Pekka Hukka baada ya kuwasilisha hati za utambulisho akiongea na Rais Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam leo Septemba 9, 2015.
Balozi mpya wa Finland nchini Bw. Pekka Hukka akipigiwa nyimbo za taifa baada ya kuwasilisha hati za utambulisho kwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam leo Septemba 9, 2015.
Balozi mpya wa Sweden Bi. Katrina Rangnitt nchini akiweka saini kitabu cha wageni kabla ya kuwasilisha hati za utambulisho kwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam leo Septemba 9, 2015.
Balozi mpya wa Sweden nchini Bi. Katrina Ranngitt  akiwasilisha hati za utambulisho kwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam leo Septemba 9, 2015.
Balozi mpya wa Sweden nchini Bi. Katrina Ranngitt  akisalimiana na Naibu Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa baada ya kuwasilisha hati za utambulisho kwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam leo Septemba 9, 2015.
Balozi mpya wa Sweden nchini Bi. Katrina Ranngitt akiwa katika mazungumzo na  Rais Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam leo Septemba 9, 2015.
Balozi mpya wa Sweden nchini Bi. Katrina Ranngitt akisindikizwa na Mnikulu wa Ikulu Bw. Jumaa Bwambo  baada ya kuwasilisha hati za utambulisho kwa Rais Jakay Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam leo Septemba 9, 2015.

Na Beatrice Lyimo-Maelezo
9/9/2015
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amepokea hati za utambulisho wa  mabalozi wanne kutoka nchi  nne kwa nyakati  tofauti, ambao wanaziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Halfa hiyo ilifanyika leo Ikulu jijini Dar es salaam ambapo Rais Kikwete alimpokea  mhe. Balozi  Florence Tinguely kutoka Uswis, ambaye alikuwa  wa kwanza kuwasili, wa pili kuwasili ni mhe. Balozi Yasemin Fraip kutoka Uturuki, na watatu ni  mhe. Balozi Pekka Hukka anayeiwakilisha Finland pamoja na Katarina Rangnitt anayeiwakilisha Sweden.

Mabalozi hao waliwasili Ikulu kwa nyakati tofauti, ambapo wa kwanza  aliwasili kuanzia majira ya saa 5:00 asubuhi na hafla hiyo ilimalizika majira ya saa 7:00 mchana.

Katika hatua nyingine, Rais Kikwete amemkabidhi  Bwana. Haroub Soud Mzee ambaye ni mlemavu wa miguu bajaji itakayomsaidia katika shughuli zake mbalimbali za kimasomo.

Mzee ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu katika Chuo  Kikuu cha Kampala nchini kutoka fani ya uhasibu amekabidhiwa bajaji hiyo yenye namba za usajili MC 835 AVU.

Mzee amemshukuru   Rais Kikwete  kwa usikivu wake na kujali kusikiliza na kufanikisha ombi lake lililochukua muda wa miezi mitatu tangu alipowasilisha.

Kwa upande wake Mwandishi Msaidizi wa  Rais  Bi. Premi Kibanga amesema kuwa Rais anapokea maombi mbalimbali ya vitu tofauti kutoka kwa wananchi na kujitahidi kufanikisha na kutatua shida zinazowakabili. 

No comments:

Post a Comment