TANGAZO


Saturday, September 12, 2015

Rais Jakaya Kkikwete atunuku Kamisheni kwa Maofisa Wanafunzi 166 katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli

Amiri Jeshi Mkuu Dkt.Jakaya Mrisho akiwa katika gari maalum la wazi na Mkuu wa Chuo cha maafisa wa Jeshi(TMA) Monduli akiingia katika uwanja wa paredi tayari kwa kutunuku kamisheni kwa maafisa wapya wa jeshi leo. (Picha zote na Freddy Maro)
Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Adolf Mwamunyange akimkaribisha Amiri Jeshi mkuu Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika chuo cha jeshi Monduli (TMA) ili kutukunu kamisheni kwa maafisa wapya leo.  
Maofisa wapya wa Jeshi wakila kiapo mbele ya Amiri jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete. 
Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Adolf Mwamunyange akimkabidhi moja ya zawadi Amiri Jeshi mkuu Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika chuo cha jeshi Monduli(TMA) ili kutukunu kamisheni kwa maafisa wapya leo.  
Amiri Jeshi Mkuu Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi katika Cho cha Jeshi(TMA) Monduli Mkoani Arusha leo. 
Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange akimkabidhi Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete zawadi ya picha akiwa katika gari la wazi katika sherehe za awali chuoni hapo, na kitara pamoja na nembo maalum ya jeshi kwa kutambua mchango wake katika kuliboresha na kulifanya la kisasa Jeshi la Wananachi wa Tanzania wakati wa Sherehe za kutunuku l\kamisheni kwa maafisa wapya wa jeshi katika chuo cha jeshi Monduli leo.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia michoro ya majengo ya chuo hicho.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiiangalia picha ya kuchora ya Mkewe Mama Salma Kikwete aliyoipokea kwa niaba yake.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride muda mfupi kabla ya kutunuku Kamisheni kwa Maofisa wapya wa Jeshi katika Chuo cha Jeshi Monduli leo. 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpa zawadi Afisa mwanafunzi bora Luteni Usu Antony Shija wakati wa sherehe za kutunuku kamisheni kwa maafisa wapya leo katika chu cha jeshi TMA Monduli leo. 
Amiri Jeshi Mkuu Rasi Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitoa akimpa zawadi afisa mwanafunzi bora wa kike Luteni Usu Martina James Shija  wakati wa sherehe za kutunuku kamisheni kwa maafisa wapya wa jeshi katika chuo hca jeshi Monduli leo.


Na Richard Mwangulube na  Wankyo Gati, TMA, Monduli
RAIS Jakaya Mrisho Kikwete  na Amri Jeshi Mkuu leo ametunuku  Kamisheni  ya lutein Usu kwa  Maofisa Wanafunzi 166    wa Kozi ndefu  katika Chuo  cha Mafunzo cha Kijeshi TMA Monduli
Kati ya wahitimu  hao  pia  wamo  maofisa wanawake 21 ikiwa ni kozi ya 56  iliyoanza mwaka 2014
Tangu aingie madarakani mwaka 2005 Rais Kikwete na Amiri Jeshi Mku  ameweza kutunuku  Kamisheni Makundi 18  ambapo  maofisa wanafunzi 3,000 wakiwemo wanawake 132  wamehitimu mafunzo katika chuo hicho.

Mbali na kutunuku Kamisheni kwa maofisa wanafunzi hao Rais Kikwete  pia ametoa zawadi kwa maofisa wanafunzi  wanne waliofanya vizuri wakati wa mafunzo hayo.

Maofisa wanafunzi waliotunukiwa zawadi na Amri Jeshi Mkuu ni  Anton Shija  alipata zawadi kwa kuwa mshindi wa Jumla wakati wa Kozi hiyo, Sharma Aman Mbegu aliyepata zawadi kwa kuwa mshindi katika masuala ya taaluma.

Aidha Rais Kikwete pia ametoa zawadi kwa  afisa mwanafunzi  Nuru  Joseph Mhama ambaye ni mshindi katika masuala ya medani za kivita na upande wa  wanawake Amiri Jeshi Mkuu  ametoa zawadi kwa  afisa mwanafunzi  Amartina  James Simba

Rais Kikwete ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama awali alikagua gwaride  la wahitimu hao lililoundwa na Gadi  nne  ambapo wahitimu hao pia walikula kiapo cha utii kwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu baada ya kupitia mbele ya Rais kwa mwendo wa pole na wa haraka.

Hii ni  sherehe yake ya mwisho kabla  kipindi cha Urais Kumalizika Oktoba mwaka huu ambapo  mwaka 1992  Rais Kikwete aliwahi kuwa Kamisaa  katika Chuo hicho cha TMA.

Sherehe hizo pia  zimehudhuriwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali  Davis Adolf  Mwamunyange, Mnadhimu  Mkuu Luteni Jenerali Samwel Ndomba, Waziri wa Ulinzi Dkt Hussein Ali Mwinyi. NA Aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi Mirisho  Sarakikya Sherehe hizo pia zimehudhuriwa na Waziri  Mkuu  Mizengo Kayanza Pinda.

Aidha  Sherehe hizo Pia zimehudhuriwa na Wakuu wa  Vyuo vya Kijeshi kutoka nchi za Afrika ya Mashariki (EAC)  za Uganda, Kenya, Rwanda na Burundi  na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue.

Wakati wa Sherehe hizo  uongozi  wa chuo ulimtunuku zawadi mbalimbali  kwa kutambua mchango wake kwa chuo hicho  yeye na mama Salma Kikwete ambapo mkozi hiyo imehusisha  maofisa wanafunzi wote kutoka Tanzania.

No comments:

Post a Comment