TANGAZO


Tuesday, March 10, 2015

Real Madrid , Schalke 04 uwanjani UEFA

Schalke 04 na Real Madrid zilipokutana katika mechi ya mkondo wa kwanza
Michuano ya Klabu Bingwa barani ulaya leo unaendelea ambapo FC Porto ya Ureno itamenyana vikali na FC Basel ya Uswis.
Katika mechi ya awali timu hizo zilitoka sare ya goli moja kwa moja.
Mechi nyingine ya kukata na shoka ya michuano hiyo hii leo itakuwa ni kati ya Real Madrid ya Hispania v Schalke 04 ya Ujerumani.
Real Madrid wana nafasi kubwa ya kusonga mbele kwani katika mechi ya awali waliifunga Schalke 04 , nyumbani kwao 2 -0.

No comments:

Post a Comment