TANGAZO


Sunday, March 15, 2015

Man United kumkosa Di Maria

Manchester United kumkosa nyota wake Angel Di Maria
Kilabu ya Manchester United itamkosa Angel Di Maria,ambaye anahudumia mafuruku ya mechi moja baada ya kupewa kadi nyekundi dhidi ya Arsenal,naye Jonny Evans akiwa anahudumia marufuku.
Mshambuliaji nyota Robbin Van Persie bado anauguza jeraha huku Marcos Rojo akiwa hajulikani iwapo atachezeshwa kutokana na jeraha la paja.
Hatahivyo Ashley Young atacheza licha ya kujiumiza mguu siku ya jumatatu.
Kocha wa kilabu ya Tottenham Mauricio Pochettino ana kikosi chake kizima.
Danny Rose huenda akacheza mechi ya leo katika safu ya ulinzi wa kushoto huku Mousa Dembele pia akitarajiwa kuanza.

No comments:

Post a Comment