Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele akiwaelekeza vijana wa Mbarali namna ya kuandika andiko la mradi wakati wa semina ya Ujasiriamali, Ujuzi, Stadi za Maisha na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana iliyotolewa kwa vijana wa Mbarali hivi karibuni.
Mwenyekiti wa Kikundi cha Wood Works Bw. Stafford Gwimile (wa pili kulia), akizungumza na maafisa kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo walipotembelea mradi wa kikundi hicho kwa ajili ya kutathmini shughuli za vijana na utoa ushauri kwa vijana wa Wilaya ya Mbarali Mkoa wa Mbeya.
Maafisa kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo pamoja na vijana wa Kikundi cha Umati Sanaa Group wakiburudika na muziki uliokua ukitumbuizwa na vijana wa kikundi hicho wakati wa ziara ya kutembelea vikundi vya vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Mkoa wa Mbeya.
Mwezeshaji kutoka
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa (waliokaa
kushoto) akizungumza na vijana wa Umati Sanaa Group wanaofanya kazi za sanaa
walipofika kuangali kazi zinazofanywa na kikundi hicho wakati wa ziara ya
uhamasishaji kwa vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Mkoa wa Mbeya. (Picha
zote na Genofeva Matemu– Mbarali, Mbeya)







No comments:
Post a Comment