Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba akijibu maswali wakati wa kipindi cha Maswali na Majibu Bungeni leo.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne Kilango Malecela akijibu maswali ya wabunge.
Baadhi ya Mawaziri wakiwa kwenye ukumbi wa Bunge jana.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara akiteta jambo na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Juma Nkamia Bungeni mjini Dodoma.
Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Diana Chilolo akiuliza swali la nyongeza kwa Waziri wa Katiba na Sheria kuhusu Mahakama ya Wilaya ya Iramba mkoni Singida.
Mbunge wa Mwibara (CCM), Kangi Lugola akichangia taarifa za kamati zilizowasilishwa leo Bungeni mjini Dodoma.
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Stephen Wassira (kulia) akijadili jambo na wabunge wenzake baada ya kuahirishwa kikao cha asubuhi Bungeni mjini Dodoma leo.Wengine kutoka kulia ni Mbunge wa Maswa Magharibi (CHADEMA), John Shibuda, Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Rashid akijadili jambo na Mbunge wa Kuteuliwa Margaret Sitta, nje ya ukumbu wa Bunge.
Naibu Waziri wa Fedha Adam Malima akizungumza na Mbunge wa Singida Mjini, Mohamed Dewji baada ya Bunge kuahirishwa leo asubihi. (Picha zote na Hussein Makame-MAELEZO,
Dodoma)
Mapambano dhidi ya ujangili nchini yaonesha mafanikio makubwa
Na Hussein Makame-MAELEZO, Dodoma
KAMATI ya
Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira imesema kuwa hatua za Serikali za kupambana
na ujangili nchini zimeonesha mafanikio makubwa.
Akitoa
taarifa ya Utekelezaji wa Kazi za Kamati, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, James Lembeli
alisema kuwa pamoja na mafanikio mengine hatua hiyo imefanikiwa kukamata silaha
2000.
Alisema hadi
kufikia mwaka 2013, hali ya ujangili wa tembo ilikadiriwa kufikia tembo 30 kwa
siku, lakini Serikali ilichukua hatua ya kuzuia na kutokomeza uhalifu huo kwa
kuanzisha Operesheni Tokomeza.
“Pamoja na
madhara yalijitokeza operesheni hiyo ilisaidia kuanza kupungua kwa kesi za
ujangili wa tembo nchini” alisema Lembeli.
Alifafanua
kuwa baada ya Operesheni hiyo Serikali iliendelea kuchukua hatua zaidi kwa lengo
la kutokomeza kabisa tatizo hilo.
“Hatua
zilizochukuliwa ni pamoja na kuajiri askari wa wanyamapori zaidi ya 500 na
wengine 300 waliajiriwa ikiwa ni askari wa kujitolea”alisema.
Hata hivyo
aliishauri Serikali kuendelea na harakati za kupambana kwa nguvu zote na
ujangili na kuweka wazi hali ya ujangili
nchini ili wananchi na wadau wa hifadhi nchini waungane na Serikali.
Naye Naibu
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba alisema hatua
kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya kampuni ya simu inayotoza gharama za
maunganisho zaidi ya zile zinazodhibitiwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
(TCRA).
Naibu Waziri
Makamba alisema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Mbozi Magharibi, David
Silinde lililotaka kujua kwa nini kampuni moja inawatangazia wananchi kutoza
gharama walizotumia.
Alisema TCRA
inasimama ipasavyo kudhibiti huduma za mawasiliano kulingana na sheria zilizopo
ikiwa ni pamoja na kudhibiti hujuma mbalimbali zinazofanywa na kampuni za simu.
Alifafanua
kuwa katika kuimarisha udhibiti pamoja na hujuma hiyo, Kitengo Maalum
kimeanzishwa ndani ya TCRA kinachoshughulika na malalamiko ya wateja yanayohusu
huduma za mawasiliano.
Serikali kuondolewa wananchi changamoto za upatikanaji wa viza
Na Lorietha Laurence- Maelezo Dodoma
02/02/2015
SERIKALI ya Tanzania
inafanya jitihada za kuhakikisha kuwa inaondoa usumbufu wa upatikanaji wa viza
za Uingereza na nchi nyingine ili kupunguza changamoto zinazowakumba wananchi
wakati wa kuomba viza hizo.
Hayo yamesemwa na Naibu
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mahadhi Juma Maalim, wakati
akijibu swali la mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi, Jaku Ayoub aliyetaka
kujua kauli ya Serikali kwa wananchi wanaopata usumbufu wakati wa kuomba viza za
Uingereza.
Alisema Wizara yake
inaendelea kuzisihi nchi hizo kulegeza masharti yao ya viza kwa Watanzania ili
wananchi wa Tanzania waendelee kufaidika na uhusiano mzuri uliopo.
Alitoa wito kwa wananchi wenye dhamira ya kwenda Uingereza
kufanya maombi ya viza mapema ili kuepuka usumbufu unaojitokeza pale
wanapohitaji kusafiri.
Alibainisha kuwa Ubalozi
wa Uingereza nchini haujafungwa ingawa
huduma za viza zinatolewa kupitia wakala ambapo utaratibu wa
upatikanaji wake ni ndani ya siku 18.
“Napenda kulihakikishia Bunge lako tukufu kuwa, Serikali inaendelea kufanya jitihada
kuhakikisha usumbufu wa upatikanaji wa viza za Uingereza na nchi nyingine
unapungua kwa kiasi kikubwa” alisema Waziri Maalim.
Kuhusu mchango wa
uamuzi wa Tanzania kuwa na Ubalozi nchini Uingereza, Naibu Waziri Maalim
alisema uamuzi huo umesaidia kukuza uhusiano wa kidiplomasia na Uingereza.
“Uhusiano ambao
umetuwezesha kushirikiana katika nyanja za Elimu, Biashara, Utalii na
Uwekezaji.
Wanafuzni wa Tanzania wamekuwa wakinufaika na ufadhili wa Serikali ya Uingereza katika mafunzo ya Elimu ya Juu hususani Shahada za Uzamili na Uzamivu” alisema.
Wanafuzni wa Tanzania wamekuwa wakinufaika na ufadhili wa Serikali ya Uingereza katika mafunzo ya Elimu ya Juu hususani Shahada za Uzamili na Uzamivu” alisema.
Aliongeza kuwa Sera ya
Mambo ya Nje ya Kidiplomasia na uchumi
inaendelea kutangaza fursa za uwekezaji
zilizopo nchini ikizingatiwa kuwa
Uingereza ni mdau mkubwa katika
kuchangia bajeti ya taifa kupitia
misaada mbalimbali wanayoitoa kupitia
umoja wa Ulaya.













No comments:
Post a Comment