Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Godfrey Zambi akitoa kauli ya Serikali kuhusu Mkakati wa Serikali wa Kutatua Changamoto za Soko la Sukari nchini, leo Bungeni mjini Dodoma.
Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa (kushoto) akiteta jambo na Mbunge wa Kuteuliwa na Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, leo Bungeni mjini Dodoma.
Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Ester
Bulaya akichangia hoja ya ya Kamati za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC),
Kamati ya Bajeti na Kamati Hesabu za Serikali za Mitaa(LAAC) jana Bungeni mjini
Dodoma.
Baadhi ya wageni waliohudhuria
kwenye ukumbi wa Bunge la Jamhuri jana bungeni mjini Dodoma. (Picha zote na Hussein Makame-Maelezo, Dodoma)
Na Lorietha Laurence-
Maelezo Dodoma
SERIKALI imeandaa mikakati mbalimbali ya kuboresha afya ya wanawake wajawazito ili kupunguza
vifo vitokanavyo na uzazi.
Akijibu swali kwa Niaba
ya Waziri wa Afya na Ustawi, katika kipindi cha maswali na majibu Bungeni mjini
Dodoma, Naibu Waziri wa Maendeleo ya
Jamii Jinsia na Watoto, Dkt. Pindi Chana amesema moja ya mikakati hiyo ni mpango mkakati ulioboreshwa wa kuendeleza
kasi ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi
uliozinduliwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
Jakaya Kikwete mwaka 2014.
Alisema kuwa mpango huo
unawashirikisha wadau mbalimbali ambao ni World Lung Foundation, Plan
International, Care International, Jhpiego, UNFPA na GIZ wanaochangia katika kupanua vituo vya afya ,kujenga vyumba vya upasuaji na ununuzi
wa vifaa na tiba.
“Mkakati huu ni jitihada za serikali katika kuhakikisha
afya ya mama na mtoto inaboreshwa kwa kukomesha vifo vitokanavyo na uzazi na watoto walio chini ya umri wa miaka mitano”
alisema Dkt. Chana.
Alifafanua kuwa Rais Dkt
Kikwete ameagiza wakuu wa mikoa
kusimamia masuala ya afya kwa ngazi zote
zinahusu afya ya mama na mtoto na kuhakikisha wanawasilisha taarifa za
maendeleo ya utekelezaji kila baada ya miezi mitatu(3).
Mpango mkakati huo
umeanzishwa kutokana na bajeti finyu ya afya ya mama na mtoto ambayo imekuwa ikipungua
kila mwaka wa fedha , hivyo serikali ikaona umuhimu wa kuangalia
njia mbadala ya kuweze kupata fedha ili
kuongeza bajeti.









No comments:
Post a Comment