Kocha wa kilabu ya Manchester United Louis Van Gaal amewaambia wachezaji wa zamani wa kilabu hiyo Gary NevilLe na mwenzake Paul Scholes kwamba hawajui chochote kinachoendelea katika kilabu hiyo.
Van Gaal anaiongoza timu yake katika mechi ya jumapili dhidi ya mabingwa wa zamani wa ligi ya EPL Liverpool huku Neville akisema kuwa Manchester United inalinda lango lake kama kilabu ya walevi naye Scholes akisema kuwa anahofia kwamba wachezaji chipukizi katika eneo la kazkazini mashariki mwa Uingereza huenda wakaelekea katika uwanja mpya wa kilabu ya Manchester City.
Lakini kocha Van Gaal alimjibu Neville wiki iliopita akimuonya kujihadhari na matamshi yake.'



No comments:
Post a Comment