TANGAZO


Wednesday, December 31, 2014

Mtoto zeru zeru atekwanyara Tanzania


Mazeru zeru Tanzania

Polisi nchini Tanzania wanasema kuwa wamewakamata watu wanne kutokana na kutekwa nyara kwa msichana mmoja zeruzeru.
Msichana huyo wa miaka 4, Pendo Emmanuelle Nundi alitekwa siku ya jumamosi kutoka nyumbani kwao katika jimbo la kazkazini la Mwanza.
Msemaji wa Polisi Valentino Mlowola amesema kuwa babaake mtoto huyo ni miongoni mwa wanaochunguzwa ,ili kujaribu kujua iwapo bado yuko hai.
Utafiti wa Umoja wa Mataifa unasema kuwa takriban mazeruzeru 74 wameuawa nchini Tanzania ambapo vipande vya miili yao huuzwa kama vivutio vya bahati kwa takriban dola mia sita.

No comments:

Post a Comment