TANGAZO


Saturday, September 20, 2014

Serikali ya Ukraine na waasi waafikiana


Rais za zamani wa Ukraine kushoto Leonid Kuchma
Rais wa Zamani wa Ukraine amesema kuwa mpango wa amani umeafikiwa katika mazungumzo yanayolenga kusitisha mgogoro unaoendelea mashariki mwa Ukraine.
Leonid Kuchma amesema kuwa mpango huo unahusisha kuwekwa kwa eneo la kilomita 30 ambalo halitakuwa na majeshi kati ya mpaka wa ukraine na Urusi,kuondolewa kwa vikosi vya kigeni mbali na kupigwa marufuku kwa ndege za kijeshi zinazopaa katika eneo moja la anga ya mashariki mwa Ukraine.
Bwana Kuchma amekuwa akifanya mazungumzo nchini belarus na wapiganaji wanaounga mkono Urusi ,balozi wa Urusi mjini Kiev Mikhail Zurabov pamoja na mjumbe kutoka shirika la usalama wa muungano wa ulaya.
Makubaliano ya kusitisha vita yalioafikiwa kati ya Ukraine na waasi hao mapema mwezi huu yamepunguza ghasia mashariki mwa Ukraine ,lakini kumekuwa na ripoti za ufyatulianaji wa risasai wa mara kwa mara na urushaji wa makombora kutoka pande zote mbili.

No comments:

Post a Comment