TANGAZO


Thursday, May 22, 2014

Wasanii wa Muziki nchini watarajia kushiriki sherehe za Fiesta Congo


Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akizungumza na ujembe wa watu kutoka Congo hawapo pichani waliomtembelea ofisini kwake kuwaalika wasanii kutoka Tanzania kushiriki katika sherehe za fiesta nchini Congo kwa lengo la kudumisha amani na mshikamano katika nchi za maziwa makuu. Kulia ni Mwenyekiti wa sherehe za fiesta kutoka Congo Bi. Anne Gizenga.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akifafanua jambo kwa wajumbe wa maandalizi ya fiesta kutoka Congo walipomtembelea ofisini kwake, kulia ni mratibu wa sherehe za fiesta kutoka Congo Bw. Faso Mushigo Celestin na katikati ni Mwenyekiti wa sherehe za fiesta kutoka Congo Bi. Anne Gizenga.
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara wapili kushoto akipokea zawadi kutoka kwa wajumbe kutoka Congo waliokuja nchini kuwaalika wasanii wa Tanzania kushiriki fiesta nchini Congo, kushoto ni Mkurugenzi Idara ya Utamaduni Profesa Hermas Mwansoko.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akiangalia CD iliyorekodiwa matukio mbalimbali ya fiesta ya mwaka jana ilivyokuwa nchini Congo. Kulia ni  Mwenyekiti wa sherehe za fiesta kutoka Congo Bi. Anne Gizenga. (Picha zote na Genofeva Matemu – Afisa Mawasiliano Serikalini WHVUM)

No comments:

Post a Comment