Ripoti kutoka Musumbiji zinaarifu kuwa wanaharakati waliojihami
kutoka kundi la upinzani la Renamo,wameshambulia kituo kimoja cha polisi katika
mji wa kati wa Maringue.
Renamo ilikaidi makubaliano hayo baada ya vikosi vya serikali kushambulia kambi iliokuwa na kiongozi wake Afonso Dhlakana na kumlazimu kutoroka.
Hali ya wasiwasi kati ya serikali na Renamo imeongezeka katika siku za hivi karibuni huku mapigano yakiripotiwa katika maeneo mbalimbali.
Inakadiriwa kwamba zaidi ya watu milioni moja waliuawa katika vita hivyo vya miaka 16 vilivyosababisha mazungumzo ya amani huku Renamo ikibadilika kutoka kundi la wanamgambo hadi chama cha kisiasa.
No comments:
Post a Comment