TANGAZO


Thursday, April 18, 2013

Rais Kikwete awaongoza waombolezaji mazishi ya Bi. Kidude, kisiwani Unguja

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, alipohudhuria nyumbani kwa Marehemu, Bi. Fatma binti Baraka 'Bi. KIDUDE', kuhani kwa familia ya marehemu huyo leo asubuhi, Rahaleo mjini Unguja. (Picha zote na Ramadhan Othman, Ikulu, Othman Maulid wa ZanZinews)

Waombolezaji akinamama mbalimbali, waliofurika katika maziko ya Msanii Maarufu wa muziki wa tarab ya asili, Marehemu Bi. Fatma Binti Baraka 'Bi. KIDUDE', huko nyumbani kwake Rahaleo, Mjini Unguja.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la mapinduzi, Dk.
Ali Mohamed Shein (wa nne  kulia), akijumuika na viongozi na waislamu katika kumswalia marehemu msanii maarufu wa muziki wa tarab ya asili, Fatma Binti Baraka 'Bi. Kidude' katika msikiti wa Mwembeshauri, Mjini Unguja leo.

Maelfu ya wananchi na waislamu waliofurika katika msikiti wa Mwembeshauri, wakilibeba jenenza lenye mwili wa masanii maarufu wa muziki wa tarab ya asili nchini, marehemu Fatuma Binti Baraka 'Bi. Kikidude leo, wakati wa maziko yake, kijini kwao Kitumba, Wilaya ya Kati Unguja.

Vijana waliobeba Jeneza lenye mwili wa Marehemu Msanii
maarufu wa muziki wa tarab ya asili, Fatma Binti Baraka 'Bi. Kidude' wakati wa maziko yake yaliyofanyika leo, huko kijijini kwao  Kitumba, Wilaya ya Kati Unguja, ambapo maziko yake yamehudhuriwa na wasanii mbali mbali ndani na nje ya nchi. 



Waombolezaji wakilebeba jeneza lenye mwili wa marehemu Bi. Kidude wakati wa mazishi yake kijijini kwao, 
Kitumba, Wilaya ya Kati Unguja.

Baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya wakiwa katika mazishi ya msanii huyo.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad na wa Pili, Balozi Seif Ali Idd, wakisoma hitma wakati wa kuomboleza kifo cha msanii maarufu wa muziki wa tarab ya asili, Bi. Kidude Binti Baraka leo.





Waombolezaji wakisoma hitma wakati wa maombolezo hayo leo.








Waombolezaji wakiitoa maiti ya Bi. Kidude kwa ajili ya 

kuizika kijijini kwao Kitumba, Wilaya ya Kati, Unguja.

Baadhi ya Wananchi waliohudhuria katika maziko ya
marehemu Bi Fatma Baraka (Kidude)  kijijini kwao Kitumba, 

Wilaya ya Kati Unguja.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la mapinduzi, Dk 

Ali Mohamed Shein (kulia), Rais wa  Jamhuri ya Muungano, 

Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, Makamo wa Kwanza wa Rais 

Zanzibar, Maalim Seif Sharif na Makamo wa Pili wa Rais, 

Balozi Seif Ali Iddi, wakiitikia dua baada ya maziko ya Msanii 

maarufu wa muziki wa tarab ya asili, Fatma Binti Baraka 'Bi. 

Kidude', aliyefariki jana na kuzikwa leo, kijijini kwao, 

Kitumba, Wilaya ya Kati, Unguja.

No comments:

Post a Comment