Baadhi
ya Watoto wakibeba mabango yenye
ujumbe tofauti
unaosisitiza kulindwa haki zao, wakipita kwa maandamano mbele
ya Mgeni rasmi, Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein katika sherehe za
uzinduzi wa
Mradi wa "ONE WORLD FOOTBALL FOR AFRICA",
zilizofanyika leo, Uwanja wa Amaan Studiuam, ikiwa ni
shamrashamra za maadhimisho ya Miaka 49 ya Mapinduzi
ya Zanzibar. (Picha zote na Ramadhan Othman, Ikulu)
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali
Mohamed Shein, akiwapungia mkono Vijana waliopita mbele ya
jukwaa
la Uwanja wa Amaan, wakati akipokea maandamano ya
vijana katika
sherehe za uzinduzi wa Mradi wa "ONE WORLD
FOOTBALL FOR AFRICA",
ikiwa ni katika shamrashamra za
Miaka 49 ya maadhimisho ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kulia
ni
Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na MIchezo Said Ali
Mbarouk
Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na MIchezo Said Ali
Mbarouk
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali
Mohamed Shein, akitia saini Mpira katika uzinduzi wa Mradi wa
"ONE WORLD FOOTBALL FOR AFRICA", mradi ambao
utawapatia vijana wa Zanzibar Mipira Ishirini Elfu (20,000), katika
vikundi mbalimbali na kupelekea kuongezeka kwa vipaji vya Soka
nchini, katika shamrashamra za kuadhimisha miaka 49 ya
Mapinduzi ya Zanzibar.
Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali
Mohamed Shein, akimkabidhi tuzo mmoja wa wawakilishi wa
Mashirika yaliyosaidia kufanikisha mradi huo.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk.Ali
Mohamed Shein,akimkabidhi zawadi Mwakilishi wa Shirika
la
UNICEF Paulo Edwards, katika sherehe za uzinduzi wa Mradi wa
ONE WORLD FOOTBALL FOR AFRICA", katika Uwanja wa
Amaan, ikiwa
ni shamra shamra za Miaka 49 ya Mapinduzi
Matukufu ya Zanzibar.

No comments:
Post a Comment