TANGAZO


Monday, January 7, 2013

Rais Dk. Shein azindua Shule ya Umoja Uzini Sekondari, Wilaya ya Kati Unguja


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa Shule ya Umoja ya Sekondari ya Uzini, Wilaya ya Kati Unguja, katika shamrashamra za kilele  cha miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akifungua pazia kama ishara ya uzinduzi wa Shule ya Umoja Uzini Sekondari, Wilaya ya Kati Unguja, katika  shamrashamra za kilele  cha miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kulia ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Ali Juma Shamuhuna. (Picha zote na Ramadhan Othman, Ikulu)
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (wa tatu kulia), akifuatana na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Umoja ya Uzini Sekondari, Yussuf Ali Mohamed (wa pili kulia), alipokuwa akitembelea sehemu za vyumba vya kusomea katika shule hiyo, baada ya kuifungua rasmi leo, ikiwa ni shamrashamra za kilele cha miaka 49 ya Mapinduzi  ya Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (wa tatu kushoto), akipata maelezo kutoka kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Umoja Uzini, Yussuf Ali Mohamed (katikati), wakati alipotembelea moja ya darasa la kusomea baada ya kuifugua rasmi shule hiyo leo, ikiwa ni shamrashamra za kilele cha miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (katikati), akipata maelezo kutoka kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Umoja Uzini, Yussuf Ali Mohamed (kushoto), wakati alipotembelea darasa la Kompyuta baada ya kuifungua rasmi Shule hiyo leo, ikiwa ni shamrashamra za kilele cha miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Wapili kulia ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Ali Juma Shamuhuna

No comments:

Post a Comment