Ofisa Masoko wa Benc ABC, Evelyne Auguste akizindua
mtandao wa http://www.ligikuu.co.tz/ , utakao toa habari za Ligi Kuu ya Vodacom, uliozinduliwa leo, Hoteli ya
JB Belmonte, jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia katika picha wanaoshuhudia tukio
hilo, ni Rodney Rugambo, Meneja Masoko wa Push Mobale, Wawila Nzowa, Meneja
Maendeleo ya Biashara wa Kampuni ya Lajann E Systems na kushoto ni Dennis Rauya,
Meneja wa BencABC, tawi la Quality Centre jijini Dar es Salaam na Salum
Mwalimu, Meneja Mawasiliano wa Vodacom.
Kutoka kulia ni Rodney Rugambo, Wawila Nzowa, Evelyne
Auguste na Dennis Rauya wakifuatilia maelezo ya mmoja wa wataalam wa mtandao huo,
wakati wa uzinduzi wake.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika
uzinduzi wa mtandao huo.
Ofisa Masoko wa Benc ABC, Evelyne Auguste akitoa
maelezo juu ya udhamini wa benki hiyo, kwa mtandao wa Ligi Kuu.
Rodney Rugambo, Meneja Masoko wa Push Mobile,
akizungumzia kuhusu udhamini wa kampuni hiyo kwa mtandao huo ili kuboresha mchezo wa
mpira wa miguu hapa nchini .
Meneja Mawasiliano wa Vodacom, Salim Mwalim akiishukuru
Kampuni hiyo kwa kuanzisha mtandao huo, ambao amesema utasaidia sana kutangaza
mpira wa miguu nje ya nchi na kuwatangaza wachezaji wa Ligi Kuu ya
Vodacom. (Picha zote na mpigapicha wetu)






No comments:
Post a Comment