Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed shein na mkewe, mama Mwanamwema Shein, wakipokea mashada
ya maua kama ishara ya ukaribisho katika Ikulu ya Vietnam, alipofika kwa
mazungumzo na Makamo wa Rais wa Vietnam, Bibi Nguyen Thi Doan, akiwa na ujumbe
wake katika ziara rasmi ya wiki moja ya Kiserikali nchini humo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed shein, akiwatambulisha viongozi
aliofuatana nao kwa Makamo wa Rais wa Vietnam, Bibi Nguyen Thi Doan, walipowasili
Ikulu ya nchi hiyo kwa mazungumzo ya kuimarisha uhusiano na Ushirikiano baina ya
pande zote, akiwa katika ziara rasmi ya wiki moja nchini humo.
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Mama Mwanamwema Shein, akisalimiana na Makamo wa Rais wa Vietnam, Bibi
Nguyen Thi Doan, alipowasili Ikulu nchini Vietnam, akifuatana na mumuwe, Rais wa
Zanzibar katika ziara rasmi ya wiki moja ya Kiserikali chini Vietnam.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed shein, akisalimiana na Mawaziri na viongozi mbalimbali
wa nchini Vietnam alipofika Ikulu ya nchi hiyo, kwa mazungumzo na Makamo wa Rais
wa Vietnam, Bibi Nguyen Thi Doan, akiwa katika ziara rasmi ya Kiserikali nchini
humo ya wiki moja.
Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed shein, akisalimiana na Makamo
wa Rais wa Vietnam, Bibi Nguyen Thi Doan, alipowasili Ikulu nchini Vietnam, akiwa na
ujumbe wake katika ziara rasmi ya Kiserikali nchini humo ya wiki
moja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,
Dk. Ali Mohamed shein (katikati), akiwa ujumbe aliofuatana nao katika Mkutano
maalum na Uongozi wa Serikali ya Vietnam, ukiongozwa na Makamo wa Rais wa nchi
hiyo, Bibi Nguyen Thi Doan (hawapo pichani), katika ukumbi wa Ikulu,
kuimarisha Uhusiano na Ushirikiano baina ya pande mbili hizo, katika ziara rasmi
ya Kiserikali ya wiki moja.
Viongozi wa Serikali waliofuatana na Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi , Dk. Ali Mohamed Shein, wakiwa kwenye mkutano maalum na uongozi wa
Serikali ya Vietnam.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akiteta jambo na mwenyeji wake, Kiongozi Mkuu
katika Ofisi ya Rais Ikulu nchini Vietnam, Giang Son, wakiwa katika ukumbi wa
Mapunziko (VIP) katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hanoi nchini
Vietnam, akiwa na ujumbe wake katika ziara rasmi ya Kiserikali jana.
Mama Mwanamwema Shein (kulia), Waziri wa Kazi
Uwezeshaji wananchi kiuchumi na Ushirika, Haroun Ali Suleiman (katikati) na Balozi
wa Tanzania nchini China pia akiwa anafanyakazi zake nchini Vietnam, Philip
Marmo, wakiwa katika chumba cha mapumziko (VIP) katika uwanja wa ndege wa
Kimataifa wa Hanoi, nchini Vietnam, wakiwa ni miongoni mwa ujumbe wa Rais wa
Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein nchini Vietnam.
Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana
na Maofisa wa Serikali ya Vietnam, alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Hanoi, nchini Vietnam, akiwa katika ziara rasmi ya
Kiserikali ya wiki moja nchini humo.
Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (katikati), akifuatana
na mwenyeji wake, Kiongozi Mkuu katika Ofisi ya Rais Ikulu Nchini Vietnam,
Giang Son (wa pili kushoto), baada ya mapokezi rasmi katika uwanja wa ndege wa
Kimataifa wa Hanoi, nchini Vietnam, akiwa na ujumbe wake katika ziara rasmi ya
Kiserikali ya wiki moja nchini humo jana. Kushoto ni Balozi wa Tanzania, nchini China ambaye pia anawakililisha nchini
Vietnam, Philip Marmo. (Picha zote na Ramadhan Othman, Ikulu)
No comments:
Post a Comment