TANGAZO


Friday, May 18, 2012

Mawaziri Profesa Tibaijuka na Dk. Huvisa wakutana na Makamu wa Rais, Ubomoaji nyumba za fukweni

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, amekutana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa, Anna Tibaijuka na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Terezya Huvisa, kwa mazungumzo na kupokea taarifa ya zoezi la bomoa bomoa nyumba zilizojengwa maeneo ua ufukweni, ambalo linatarajia kuanza hivi karibuni. Mazungumzo hayo yalifanyika ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu Dar es Salaam jana Mei 17, 2012. Katika picha kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Veldiana Mashingia, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka (kulia), Mkurugenzi wa Mazingira, Dk. Julius Ningu na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk. Terezya Huvisa, baada ya mazungumzo hayo. (Picha zote na Muhidin Sufiani-OMR )

Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka (kushoto) na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Terezya Huvisa (wa pili kulia), mara baada ya mazungumzo yao kuhusu zoezi la ubomoaji wa nyumba zilizojengwa maeneo ua ufukweni, ambalo linatarajia kuanza hivi karibuni. Mazungumzo hayo yalifanyika ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu Dar es Salaam jana Mei 17, 2012. Kulia ni Mkurugenzi wa Mazingira, Dk. Julius Ningu.

No comments:

Post a Comment