| Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), John Cheyo (wa pili kulia) na Katibu wa Kamati ya (PAC), Ramadhan Issa Abdallah (wa pili kushoto) pamoja na baadhi ya wanakamati na watendaji wa Mkoa wa Dar es Salaam, wakiangalia orodha yenye majina ya malipo kwa waatihirika wa mabomu ya Mbagala Kuu, wakati walipowatembelea Mei 22. 2012, huko Mbagala Kuu na kuangalia maeneo ya wakazi hao, ambayo mengine yamekarabatiwa. Mwenyekiti huyo amewashauri baadhi ya waathirika hao kwenda kuchukua hundi zao haraka kabla ya zoezi la malipo kufungwa. Tukio la kulipuka kwa mabomu lilitokea mwaka 2009 huko Mbagala Kuu Mkoa wa Dar es Salaam na kusababisha maafa kwa baadhi ya wakazi. (Picha zote na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO) |
No comments:
Post a Comment