TANGAZO


Wednesday, May 23, 2012

Kamati ya Bunge ya PAC yatembelea waathirika wa Mabomu Mbagala, jijini Dar


Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), John Cheyo (wa pili kulia) na Katibu wa Kamati ya  (PAC), Ramadhan  Issa  Abdallah (wa pili kushoto) pamoja na baadhi ya wanakamati  na watendaji wa Mkoa wa Dar es Salaam, wakiangalia orodha yenye majina ya malipo kwa waatihirika wa mabomu ya Mbagala Kuu, wakati walipowatembelea Mei 22. 2012, huko Mbagala Kuu na kuangalia maeneo ya wakazi hao, ambayo mengine  yamekarabatiwa. Mwenyekiti  huyo amewashauri  baadhi ya waathirika  hao kwenda  kuchukua hundi  zao haraka  kabla ya zoezi  la malipo kufungwa. Tukio la kulipuka kwa mabomu  lilitokea mwaka 2009 huko Mbagala Kuu  Mkoa wa Dar es Salaam na kusababisha maafa kwa baadhi ya wakazi. (Picha zote na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO)

Mbunge wa Kigamboni,  Dk. Faustine Ndugulile (mwenye suti nyeusi), akiwasikiliza baadhi ya waathirika wa mabomu ambao  wamechukua hundi  zao za malipo na kuwawezesha kukarabati  makazi yao . Mbunge Ndugulile aliongozana na wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), inayoongozwa na Mwenyekiti wake John Cheyo hayupo Pichani , Mei 22.2012.

Muathirika wa mabomu ya Mbagala, yaliyotokea mwaka 2009, mkoani Dar es Salaam,  Mzee Steven  Gimongi  (kushoto), akitoa maelezo ya jinsi  alivyoathirika  mbele ya Mwenyekiti wa  Kamati ya  Hesabu za Serikali (PAC), John Cheyo (mwenye koti   katikati) pamoja na ujumbe wake,  walipotembelea  Mbagala Kuu na kuangalia sehemu hiyo pamoja na kuzungumza na waathirika  hao.

Baadhi ya waathirika wa mabomu ya Mbagala, wakiwa katika mkutano na  Kamati ya PAC – Mei 22.2012.

Mwenyekiti wa (PAC), John Cheyo (wa tatu kulia), Mbunge wa Kigamboni Dk. Faustine Ndugulile (mwenye  suti nyeusi) pamoja na Wajumbe ya Kamati ya (PAC) na baadhi ya uongozi wa watendaji wa Serikali, mkoani Dar es Salaam, wakikgua baadhi ya makazi ya waathirika wa mabomu ya Mbagala Kuu jana Mei 22.2012.

Mwenyekiti wa (PAC), John Cheyo akimwelekeza jambo, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Peniel Lyimo, wakati walipokuwa wakiwatembelea waathirika hao jana.

No comments:

Post a Comment