Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kumalizika kwa uhasma kati yao na Mkurugenzi wa Clouds Media, Rugem Mutahaba (kulia), uliomalizwa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Emmanuel Nchimbi na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lisu (hawapo pichani), Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Clouds Media, Ruge Mutahaba, akizungmza na waandishi wa habari wakati wa kuelezea kuhusu upatanishi huo. Kushoto ni aliyekuwa mgomvi wake, Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi.
Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi na Mkurugenzi wa Clouds Media Ruge Mutahaba, wakipeana mikono, Dar es Salaam leo, ikiwa ni ishara ya kupatana na kumaliza kwa tofauti zao zilizotokana na sababu za kimuziki zilizodumu kwa muda wa miaka miwili. Kushoto ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Emmanuel Nchimbi na kulia ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lisu waliopatanisha mgogoro huo.





No comments:
Post a Comment