Msajili
wa Hazina Bw. Laurence Mafuru akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari leo
jijini Dar es salaam kuhusu umiliki wa hisa za Serikali katika Shirika la Usafirishaji
Dar es salaam (UDA) na kubainisha kuwa Serikali inamiliki hisa 49% katika
shirika hilo kinyume na upotoshaji unaofanywa na baadhi ya watu kuwa Serikali
imeuza hisa zote kwa muwekezaji. Kulia ni Afisa Habari wa Ofisi ya Msajili wa
Hazina Bw. Gerald Chami. (Picha zote na Idara ya Habari, Maelezo)
Mkuu
wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Ofisi ya Msajili wa Hazina Gerald
Chami akifafanua jambo kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam wakati
wa mkutano wa Ofisi ya Msajili wa Hazina na vyombo vya habari.kushoto ni
Msajili wa Hazina Bw. Laurence Mafuru.
Baadhi
ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano wa Msajili wa Hazina leo jijini Dar
es salaam uliolenga kutoa ufafanuzi kuhusu faida za Ripoti ya Mkaguzi na
Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika kuongeza uwajibikaji na tija
kwenye utumishi wa umma hasa kwa kuzingatia mapendekezo ya ripoti ya mwaka 2014/2015.
No comments:
Post a Comment